HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, April 25, 2018

RAIS DKT.MAGUFULI ANATARAJIWA KUWA MGENI RASMI MAADHIMISHO UHURU WA HABARI NCHINI

Na Agness Francis, Blogu ya Jamii
RAIS wa Serikali ya Awamu ya Tano Dk. John Mgufuli  kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya uhuru wa habari  Nchini ambayo kitaifa yatafanyika Mkoani Dodoma  Mei 2 hadi 3  mwaka huu ikiwa ndio kilele chake na kauli mbiu inasema  ni wajibu wa Serikali vyombo vya habari haki na utawala wa sheria.

Ambapo  wageni  zaidi ya 300 wanatajiriwa kuhudhuria  hafla hiyo wakiwepo wadau , wanahabari  ,wabunge na taasisi mbalimbali ambapo kimataifa Afrika  inafanyika Nchini Ghana Accra zaidi ya nchi 100  zitawakilisha katika hafla hiyo.

Akizungumza  jjjini Dar es Salaam Mwenyekiti wa Taasisi  ya vyombo vya habari Kusini mwa Jangwa la Sahara Salome Kitomari amesema katika siku hizo watazungumzia umuhimu wa  uhuru wa habari, utawala bora kwa waandishi wa habari na  wanasheria kama Mahakama kuwa na uhuru  wa kusimamia kesi za jinai za kuwa na uwazi kwa wanahabari vilevile na kukumbusha kutekeleza majukumu katika  uandikaji wa habari kuwa sahihi.

Aidha Makamo wa Rais wa Umoja wa Klabu za waandishi wa habari Jane Mihanji amesema wao wamekuwa na jukumu la kuwaweka pamoja waandishi wa  habari  na kuwapa mafunzo na  kuwapatia  vitendea kazi.

Ametaja baadhi ya vitendea kazi hivyo ni kamera na kompyuta  ili kurahisishia majukumu yao ya kuhabarisha umma ambapo amesisitiza kutokana na uhaba wa vyumba vya habari  mikoani  inakuwa vigumu kupata stori kutoka nje ya Dr es Salaam.Hivyo amesema wamewajengea uwezo  wa mafunzo  ili kuhakikisha mazingira ya kazi yanakuwa rafiki katika utendaji.

"Tumeshuhudia stori ikiwa inatoka lakini katika kufufua maovu yanayotendeka  inaleta  misukosuko, hivyo tunaomba Serikali kuwajibika kufanya kazi yake kwenye upande wa haki na waandishi wa habari kutoa taarifa bila kupendelea mtu na kutoa chukua rushwa,"amesema Mahinja.

Mkurugenzi wa  Tanzania Media Foundation (TMF) Fausta Musokwa amesema watashirikiana na wadau wengine kwenye tasnia ya habari kuadhimisha siku hiyo umuhimu na wapo kwa ajili ya kuimarisha vyombo vya habari vinafanya kazi katika mazingira rafiki na kuhakikisha wanahabari kutoa taarifa makini zenye ubora  kwa  jamii.

Kwa upande wa Ofisa habari wa Umoja wa  Wataifa (UN) Stella Vuzo amesema kwa sasa umoja huo unatekeleza maendeleo  endelevu ifika 2030 kila nchi hupaswa kuelezea namna gani imetekeleza hilo lengo na kuhakikisha kuwepo na ushirikiano kwa wanahabari kusaidia kupata taarifa mbali mbali .
Mwenyekiti wa MISA Tanzania Bi. Salome Kitomari akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya maadhimisho ya uhuru wa habari  Nchini ambayo kitaifa yatafanyika Mkoani Dodoma  Mei 2 hadi 3  mwaka huu na kauli mbiu inasema  ni wajibu wa Serikali vyombo vya habari haki na utawala wa sheria.
Makamu wa Rais wa  Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Jane Mahanji akizungumza na waandishi wa habari namna wanavyokwenda begakwabega na waandishi kwa kuto semina ili kutoa habari zenye faida kwa Taifa.
Mkurugenzi wa  Tanzania Media Foundation (TMF) Fausta Musokwa akizungumza na waandishi wa habari wanavyochangia kwa kiasi kikubwa vyombo vya habari kwa kutoa pesa ili vyombo hivyo vijiendeshe.
Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Stella Vuzo akizungumza na waandishi wa habari kuhusuumoja wa Mataifa unavyodhamini mchango mkubwa wa waandishi wa habari wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuelekea siku ya uhuru wa vyombo vya habari hapa nchini.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad