HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, April 13, 2018

NUSU FAINALI YA LIGI YA MABINGWA BARANI ULAYA HAPATOSHI

Na Bakari Madjeshi, Globu ya Jamii
HATIMAYE yametimia, Droo ya Nusu Fainali ya Michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya imemalizika kupangwa mchana huu, kwa miamba ya soka barani humo kukutana uso kwa uso.
Real Madrid kutoka nchini Hispania itakuwa na kibarua cha kumenyana na Bayern Munich wakati Liverpool wao wakivaana na AS Roma.
Mkondo wa kwanza wa michezo hiyo inatarajiwa kupigwa kati ya April 24/25 wakati mkondo wa pili unatazamiwa kupigwa kati ya May 1/2mwaka huu.

Wakati huo huo Michuano ya UEFA Europa League, droo yake ya Nusu Fainali imemalizika mchana huu, kwa Arsenal ya Uingereza kuikabili Atletico Madrid ya Hispania na Olimpique de Marseille ya Ufaransa kuchuana na FC Salzburg.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad