HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, April 12, 2018

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA UINGEREZA HAPA NCHINI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo amekutana na kuzungumza na Balozi wa Uingereza nchini Bi. Sarah Cooke, Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu jijini Dar es Salaam.

Lengo la mazungumzo hayo ilikuwa nikuagana na Mheshimiwa Makamu wa Rais ambaye atamuakilisha Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Madola (CHOGM) utakao fanyika mjini London kuanzia tarehe 16 hadi tarehe 20 Aprili mwaka huu.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Bi. Sarah Cooke aliyefika ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Bi. Sarah Cooke mara baada ya kumaliza mazungumzo  ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiagana  na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Bi. Sarah Cooke (kulia) pamoja na Mkuu wa Masuala ya Kijamii na Siasa  Bw. Marc Thayre ofisini kwa Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) .

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad