HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, April 20, 2018

KAMPUNI YA VODACOM KUWAWEKA PAMOJA WATEJA WAKE KUPITIA HUDUMA YA IFLIX

Na Agness Francis, Blogu ya Jamii
KAMPUNI ya Simu za mkononi ya Vodacom imeamua kuwaweka pamoja wateja wake zaidi ya milioni 12 kupitia huduma ya Iflix.

Ambapo Vodacom imeingia mkataba na kampuni ya Iflix inayotoa huduma ya burudani katika nchi zinazoendelea ambapo huduma hiyo inawapa wateja wanaotumia mtandao wa Vodacom kuangalia vipindi bora duniani,sinema na vingine vingi.

Akizungumza jijini Dar es Salaam baada ya kuingia makubaliano hayo Mkurugenzi wa Kitengo cha Biashara Hashim Hendi amesema kampuni yao imedhamiria kuingiza Tanzania katika huduma ya kidigitali hasa kwa wateja wao.

Aidha Hendi amebainisha hata wasanii na waandaaji wa filamu watapata fursa ya kuuza kazi zao katika kampuni hiyo ambapo italeta kipato katika tasnia hiyo inayofanya vema hapa nyumbani na nchi za Afrika Mashariki kwa ujumla.

"Ikiwa imeshasaini zaidi ya kampuni 240 ya usambazaji duniani,Iflix inawapa watazamaji wake chaguo kubwa la vipindi vya Tv vinavyosifika pamoja na sinema zinazopendwa na mashabiki kitaifa ikiambatana na sinema kubwa za Bollywood kama vile Love Shagun,Sharafat Gayi tel lene na nyingine nyingi,"amesema Hendi.

Kwa upande wa Muandaaji wa filamu nchini Rita Paulsen amesema wanayofuraha kwa Iflix kuwatambua waandaaji wa filamu Tanzania na kuongeza hatua hiyo itasaidia kwenda na wakati.

Wakati Muanzilishi wa Iflix Britt amesema anayo furaha ya kuingia ubia na Vodacom kufikisha huduma hiyo nchini Tanzania.

"Tumedhamiria kuwapatia chaguo kubwa kabisa la vipindi vya burudani kwa uhitaji wa matakwa yao wenyewe waweze kutazama au kupakua kwenye kifaa chochote atakachopenda mteja"amesema Britt.

Ili mteja kupata huduma hiyo anatakiwa kupakua App ya Iflix bila malipo,na vifurushi maalum mteja ata bonyeza *149*01# kisha kuchagua intanenti halafu kifurushi ikifuatiwa na Iflix,kifurushi cha siku kwa Sh.1,000,cha wiki 6,500 na cha mwezi 18,000.
 Mkurugenzi kitengo cha biashara Vodacom, Hashim Hendi akizungumza katika ofisi zao Jijini Dar es Salaam mara baada ya makubaliano hayo kuhusu huduma hiyo ya Iflix inavyoweza kutoa burudani kwa wateja wao.
Mkurugenzi mkuu Iflix Britt akizungumza katika ofisi za makao makuu ya  Vodacom Jijini Dar es salaam namna na jinsi huduma hiyo katika utendaji wake wa kazi kuonyesha filamu mbalimbali pamoja na vipindi vingine vingi hapa duniani
Mwandaaji wa Filamu nchini Rita Poulsen akitoa shukrani kwa Iflix kwa kuweza kuwatambua waandaji wa Filamu Tanzani na kufikisha huduma hiyo katika ofisi za Vodacom Jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad