HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, April 6, 2018

Benki ya CRDB yakabidhi msaada wa Madarasa na Madawati kwa ajili ya wanafunzi wenye uhitaji maalum Shule ya Msingi Msasani jijini Dar

Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta pamoja na Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa, wakikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa jengo la madarasa kwa ajili ya wanafunzi wenye uhitaji maalum katika Shule ya Msingi Msasani, Dar es Salaam, Aprili 6, 2018. Msada huo ni ya sehemu ya Benki ya CRDB katika kuisaidia jamii. Ambapo Benki hiyo imejiwekea sera maalum ya kusaidia jamii ambayo inalenga kurudisha kiasi cha asilimia moja ya faida ya Benki hiyo kila mwaka, ili ziende katika shughuli za kijamii, hususani katika nyanja za elimu, afya na mazingira. Picha na Othman Michuzi.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta akizungumza na kutoa pongezi kwa Benki ya CRDB ambapo aliishukuru benki hiyo kwa msaada huo wa madarasa na madawati kwa shule ya msingi Msasani. katikati ni Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa na kulia ni Mwalimu Edward Molel.
Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa akizungumza katika hafla hiyo.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta na Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa, pamoja na wanafunzi wenye uhitaji maalum, wakimsikiliza mmoja wanalimu wa shule hiyo alipokuwa akieleza jambo kwa lugha ya alama.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta akimshukuru Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa kwa msaada huo waliotoa.
Picha ua pamoja na baadhi ya wanafunzi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad