HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, April 22, 2018

BALOZI WA TANZANIA NCHINI CHINA AZUNGUMZIA FURSA AMBAYO NCHI YETU IMEIPATA KWENYE MAONESHO YA UTALII

Na Ripota Wetu, China
BALOZI wa Tanzania nchini China Mbelwa Kairuki amesema zaidi watu 1,000 wamepata fursa ya kutembelea banda la Tanzania ambalo lilikuwepo kwenye maonesho ya utalii nchini humo.

Idadi hiyo ya watu ambao wametembelea banda la Tanzania imesaidia kuwapatia taarifa sahihi na za kutosha kuhusu utalii wetu na ni moja ya eneo ambalo limetumika vema kutangaza vivuto vilivyopo.

Balozi Kairuki ametoa kauli hiyo wakati akizungumza kwenye maoesho ya utalii yaliyofanyika nchini China ambayo yamemalizika hivi karibuni.

Akifafanua zaidi kuhusu Maonyesho ya biashara ya Utalii (China Outboard Travel & Tourism Market COTTM) yaliyomalizika hivi karibuni jijini Beijing China Balozi Kairuki amesema maonesho hayo yamekuwa na mwitikio mkubwa.

"Zaidi ya watu 1,000 wameweza kutembelea banda la Tanzania hatua ambayo imesadia watu wengi kupata taarifa za kutosha kuhusu fursa za Tanzania.Naipongeza bodi ya utalii na mamlaka zote za utalii Tanzania pamoja na mawakala wa utalii ambao walishiriki kwa lengo la kuchangamkia fursa hiyo,"amesema.

Ameogeza soko la China ni jipya na linalokua kwa kasi,hivyo matarajio yao hizo taasisi za bodi ya utalii, Hifadhi ya Ngorongoro ,TANAPA watapewa nguvu zaidi, watawezeshwa kibajeti ili wakushiriki maonyesho mengi zaidi hapa China.

"Kwasababu China ni kubwa na inayo zaidi ya majimbo 21na ni mita za mraba zaidi ya 940,000 ambayo ni kama mara kumi ya Tanzania kwa hiyo wanahitaji kuja sana hapa China ili kuwafikia watalii wengi zaidi,"amesema Balozi Kairuki.

Pia amesema "Hakuna kitu cha bure, tunapoona watalii wamekuja wengi pale nyumbani na wanatumia fedha nyingi na sisi tunafurahi kwamba sekta ya utalii imeingiza dola bilioni kadhaa, hizi namba zinatokana na kazi kubwa inayofanywa na wadau wa utalii (Bodi ya Utalii, TANAPA, hifadhi ya Ngorongoro na Makampuni mbalimbali).

"Kwa hiyo wanahitaji kuungwa mkono na wadau wote ili wafanye kazi hii kubwa zaidi ili hatimaye tufikie lengo letu la kufikia mpaka watalii 100,000 ifikapo mwaka 2020,"amesema Balozi Kairuki

Ameeleza matarajio yaliyopo mwishoni mwa mwaka huu kutaanzishwa safari za moja kwa moja za ndege kutoka Tanzania hadi China katika mji wa Guangzhou, hatua itakayochangia kukuza utalii wa Tanzania na kuwawezesha watanzania na wachina wengi kutumia ndege hiyo kwenye Shirika letu la ndege la ATCL kwa ajili ya kuja China kutalii na kufanya biashara. Wakati huohuo amefafanua kuhusu uwepo wa maoeshomakubwa Novemba mwaka huu yanayofahamika China International Import Expo (CIIE)’ kwenye Mji wa Shanghai.

"Tunataka kwenye maonyesho hayo tutangaze mambo matatu ya Tanzania kwa sababu dunia nzima itakuwa pale, kwa hiyo sisi tunataka tujikite na vitu vichache cha kwanza ni utalii, pili ni kuitangaza Tanzanite (Kutangaza madini ya Tanzanite ambayo yanapatikana Tanzania pekee).

"Wachina wengi hawayafahamu haya madini tunataka tuyatangaze wachina wayafahamu na jambo la tatu ni bidhaa za Tanzania na tungependa tupate fursa ya kutangaza kahawa, Korosho na mnvinyo wa Tanzania pamoja na bidhaa nyingine kutoka nchini kwetu,"amesema Balozi Kagaruki.

Kwa upande wa Ofisa Habari Utalii kutoka Bodi ya Utalii Tanzania Irene Mville amesema kupitia maonyesho hayo wameitangaza vilivyo nchi ya Tanzania kupitia sekta ya utalii na wanayo mategemeo makubwa ya ongezeko la wageni.

"China wamefanya kitu kizuri lakini kikubwa sana tunaishukuru Serikali ya Tanzania ambayo imewezesha ushiriki wa mashirika yake katika maonyesho hayo,"amesema Irene.

)fisa Mipango wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar Hassan Ameir Vuai ni miongoni mwa washiriki wa maonyesho hayo ambapo amesema lengo lao ilikuwa ni kutangaza vivutio vya utalii wa nchi ya Tanzania na walifanikiwa kufikia lengo.

Naye Katibu Mkuu wa Shirikisho la Wanafunzi Watanzania nchini China Remidius Emmanuel amesema mbali na maonyesho hayo,Watanzania wanaosoma nje ya nchi, endapo wataendelea kutumika kikamilifu katika kutangaza utalii na utamaduni wa nchi yetu.

"Upo uwezekano mkubwa wa kuchochea ongezeko la watalii hususani katika Taifa hili la China, maana fursa hizi katika vyuo vyetu hakuna malipo au gharama yoyote , tukiendelea kuzitumia vema fursa hizi itasaidia zaidi kuunga mkono juhudi za Serikali yetu.

Tunaishukuru sana Serikali kupitia Ubalozi wa Tanzania nchini Chin,"amesema.
Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki (Kushoto) akishiriki mahojiano maalumu yaliyolenga kutangaza Vivutio vya Utalii na Utamaduni wa  Tanzania  kupitia kituo cha runinga cha   "Chinese Satelite Travel" chenye  watazamaji zaidi ya Milioni 100 ndani na nje ya China. Mahojiano hayo yaliongozwa na Bi. Mei Qing  mtangazaji maarufu wa Television hiyo.
 Afisa Utalii kutoka Hifadhi ya Ngorongoro, Piter Makutian (Kushoto) akizungumza jambo katika  mahojiano maalumu yaliyolenga kutangaza Vivutio vya Utalii na Utamaduni wa  Tanzania  kupitia kituo cha runinga  cha   "Chinese Satelite Travel" chenye  watazamaji zaidi ya Milioni 100 ndani na nje ya China. Mahojiano hayo yalifanyika wakati wa Maonyesho ya Utalii yaliyofanyika Beijing China mapema wiki hii. Kulia ni Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki.
 Mahojiano yakiendelea  yaliyolenga kutangaza Vivutio vya Utalii na Utamaduni wa  Tanzania  kupitia kituo cha runinga  cha   "Chinese Satelite Travel"
Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki(katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa mahojiano kwenye kituo cha runinga  cha  "Chinese Satelite Travel" 
Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki(kushoto) akipata maelezo kuhusu Maonyesho ya Utalii  kutoka kwa Afisa Utalii Mwandamizi - Hifadhi ya Taifa Tarangire Theodora Aloyce (katikati), Wa pili kushoto ni Afisa Utalii habari  - Bodi ya Utalii Tanzania, Irene  Mville, Afisa Utalii- Mamlaka ya Hifadhi  ya Eneo la Ngorongoro, Piter Makutian (wa pili kulia) na Afisa Kutoka Ubalozi wa Tanzania nchini China, Lusekelo Gwassa 
 Afisa Mipango kutoka Kamisheni ya Utalii Zanzibar, Hassan Ameir Vuaiakizungumza juu ya mwenendo wa maonyesho hayo yalivyokwenda hadi kuhitimishwa
 Afisa Utalii kutoka Hifadhi ya Ngorongoro, Piter Makutian akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hitimisho la Maonyesho ya Utalii yaliyofanyika Beijing China mapema wiki hii.
Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki akizungumza na waandishi wa habari wakati wa Maonyesho ya Utalii yaliyofanyika Beijing China mapema wiki hii.
 Afisa Utalii Habari - Bodi ya Utalii Tanzania, Irene F. Mville  akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hitimisho la Maonyesho ya Utalii yaliyofanyika Beijing China mapema wiki hii.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Wanafunzi Watanzania nchini China, Remidius Emmanuel(Kushoto)  akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Compass Safari, Peter Larocque inayofanya kazi zake nchini Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad