HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, March 8, 2018

WANAWAKE WA BENKI YA TIB CORPORATE WASHEHEREKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI.


Wafanyakazi wanawake wa benki ya TIB Corporate banki ltd  wa tawi la Samora wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa kushehereka siku ya wanawake duniani.
 Siku ya Wanawake ilianza mwanzoni mwa miaka ya 1900 kwa kupitia wanawake wafanyakazi wa sekta ya viwanda nchini Marekani walioandamana kupinga mazingira duni ya kazi zao, walilalamikia ukosefu wa huduma za kijamii na kuwepo kwa vitendo vya unyanyasaji katika ajira. 
Baadaye Umoja wa Mataifa ulipaoanzishwa mwaka 1945,ilipofika tarehe 8 Machi iliridhiwa iwe Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani. Benki ya TIB wakiwa na Kauli mbiu ya "Wanawake Tunachapa kazi wakati kauli mbiu ya Taifa kwa ujumla ni

 "Kwa mwaka huu kauli mbiu ni Kuelekea Uchumi wa Viwanda tuimarishe usawa wa kijinsia na Uwezeshaji waWanawake Vijijini."
Keki ya siku ya wanawake katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani.
Kwa mwaka huu kauli mbiu ni Kuelekea Uchumi wa Viwanda tuimarishe usawa wa kijinsia na Uwezeshaji waWanawake Vijijini.
Mkurugenzi  mikopo wa benki ya TIB Corporate banki ltd, Adolphina william, meneja wa huduma kwa wateja Magreth Mulenga kwa pamoja na mteja wa benki hiyo wakikata keki kusheherekea wiki ya huduma kwa wateja katika benki yao.
Mkurugenzi  mikopo wa benki ya TIB Corporate banki ltd, Adolphina william akimlisha keki mteja wao ikiwa ni kuadhimisha siku ya wanawake duniani ambayo hufanyika kila mwaka Machi Nane.


Mkurugenzi wa hazina Bahati Minja akimlisha keki Mteja wa
benki ya TIB Corporate banki ltd ikiwa ni siku ya wanawake duinani ambayo hufanyika kila mwaka Machi nane.
Wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate banki ltd wakiwa katika picha ya pamoja  ikiwa ni kusheherekea pamoja siku ya wanawake duniani ambayo hufanyika kila mwaka Machi 8.
 Kwa mwaka huu kauli mbiu ni Kuelekea Uchumi wa Viwanda tuimarishe usawa wa kijinsia na Uwezeshaji waWanawake Vijijini.
 Meneja wa Tawi la Arusha, Juliana Mwansuva  akimlisha mteja keki ikiwa ni kuadhimisha siku ya wanawake duniani.

 Meneja wa tawi la Mbeya Lugaya Masasi katikati pamoja na maafisa huduma kwa wateja hawa Matanga na Naamini Muze ikiwa ni kusheherekea siku ya wanawake duniani.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad