MKUUWAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa
viwanda vikubwa viwili vya kuchakata pamba ambao wameahidi kununua pamba
yote itakayozalishwa nchini kuanzia msimu huu.
Viongozi
hao ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Namera Group of Industries Bw.
Hamza Rafiq Pardesi na Mkurugenzi Mtendaji wa JOC Bw. Qin Mengwei ambao
kwa pamoja wameahidi kununua pamba yote itakayozalishwa.
Waziri
Mkuu amekutana na viongozi hao leo (Jumatatu, Februari 12, 2018) jijini
Dar es Salaam na amesema kwamba wakulima waliitikia wito wa Serikali wa
kufufua zao hilo, hivyo mwaka huu wanatarajia kupata mavuno mengi.
Waziri
Mkuu amewataka viongozi hao wajiandae kununua pamba nyingi kwa sababau
mwaka huu wakulima wamelima pamba ya kutosha baada ya Serikali
kuwahamasiha waongeze uzalishaji kwa kuwa kuna soko la uhakika.
Amesema
hatua hiyo imekuja baada ya Rais Dkt. John Magufuli kutoa maelekezo ya
uhamasishaji wa kilimo hasa mazao makuu ya biashara, tayari tija imeanza
kuonekana ambapo zao la korosho limepata mafanikio makubwa na sasa
linafuatia zao la pamba.
Waziri
Mkuu amesema Serikali inashiriki kikamilifu katika usimamizi wa zao la
pamba kuanzia hatua za maandalizi ya shamba kwa wakulima kuelekezwa
kulima kitaalam, upatikanaji wa pembejeo hadi masoko, hivyo amewaalika
viongozi hao kushiriki katika mkutano utakaowakutanisha wafanyabiashara
wote wa zao hilo.
“Mimi
mwenyewe mwezi huu nitakuwa na ziara ya kikazi mkoani Mwanza, kwa hiyo
tarehe 21, Februari, nimeitisha mkutano wa wafanyabiashara wote wa pamba
nchini iwe ni wanaosokota nyuzi, kuchambua pamba au kukamua mbegu za
pamba, ili mradi wanajihusisha na pamba nanyi naomba muwepo”.
Waziri
Mkuu amesema Serikali imefurahishwa na uamuzi wao wa kutaka kununua
pamba yote itakayozalishwa nchini kuanzia msimu huu kwani ni faraja kwa
Taifa kwa sababu wakulima walipunguza uzalishaji baada ya kukosa soko la
uhakika.
Kwa
upande wao, Bw. Pardesi na Bw. Qin wamemuhakikishia Waziri Mkuu kwamba
kampuni zao zinauwezo wa kununua pamba yote inayozalishwa nchini na
kuichakata katika viwanda vyao na kutengeneza nyuzi na nguo zitakazouzwa
nchini kwa bei nafuu.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATATU, FEBRUARI 12, 2018.
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa viwanda vikubwa viwili vya kuchakata pamba cha Namera Group of Industries,na JOC. Wakurugenzi hao wameahidi kununua pamba yote itakayozalishwa nchini kuanzia msimu huu.Waziri Mkuu amekutana na viongozi hao leo, Februari 12, 2018 Ofisini kwake jijini Dar es Salaam. PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekutana na Mkurugenzi Mtendaji wa JOC Bw. Qin Mengwei (Kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Namera Group of Industries Bw. Hamza Rafiq Pardesi (kushoto mwenye miwani nyeusi) . Wakurugenzi hao wameahidi kununua pamba yote itakayozalishwa nchini Tanzania. Waziri Mkuu amekutana na viongozi hao leo, Februari 12, 2018 Ofisini kwake jijini Dar es Salaam. PICHA NA OFISI YA WAZIRI
No comments:
Post a Comment