Na Jumbe Ismailly, Singida
IDARA ya Uhamiaji Mkoa wa Singida inawashikilia kwa uchunguzi watoto wa kike watatu raia wa Rwanda wenye umri chini ya miaka 18 kwa tuhuma za kuingia nchini kinyume cha sheria.
Kaimu Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Singida,Kamishna Msaidizi, Angela Shija amesema watoto hao wenye umri kati ya miaka 9 na 13 walikamatwa Januanri 30,mwaka 2018 wilayani Manyoni.
Amesema walikuwa wakitokea nchini Rwanda wakielekea nchini Zambia kuwaona wazazi wao.
“Januari 30 mwaka 2018, ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Singida ilifanikiwa kuwakamata watoto wa kike watatu raia wa Rwanda.
"Walikamatwa wilayani Manyoni mkoani Singida wakiwa kwenye basi namba T 265 BFY mali ya Kampuni ya Katagi,” amefafanua Kamishina huyo msaidizi
Kwa mujibu wa Ofisa Uhamiaji Idara ya Uhamiaji ilifanikiwa kuwakamata watoto hao kutokana na taarifa za raia wema na watoto hao wamedai wanaelekea nchini Zambia kuwaona wazazi wao.
Hata hivyo Kamishina Msaidizi huyo wa Jeshi la Uhamiaji limeweka bayana kuwa Idara ya Uhamiaji mkoani Singida inaendelea na uchunguzi ili kubaini watu waliojihusisha na biashara hiyo ya usafirishaji wahamiaji haramu.
Aidha Kaimu Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Singida ametoa mwito kwa wananchi kujenga utamaduni wa kutoa taarifa kwenye ofisi zao au kwenye vituo vya polisi vilivyo karibu mara wanapowaona watu wasiowafahamu.
Amefafanua kuwa taarifa hizo zitaisaisi Uhamiaji kufanyia kazi za kubaini matukio ya watu wa aina hiyo na kuwachukulia hatua za kisheria.
Amesisitiza baada ya uchunguzi kukamilika na kuwabaini waliohusika katika biashara hiyo ya kuwasafirisha,na kwa sababu wana umri chini ya miaka 18,watoto hao watarudishwa nyumbani kwa wazazi wao nchini Rwanda.
IDARA ya Uhamiaji Mkoa wa Singida inawashikilia kwa uchunguzi watoto wa kike watatu raia wa Rwanda wenye umri chini ya miaka 18 kwa tuhuma za kuingia nchini kinyume cha sheria.
Kaimu Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Singida,Kamishna Msaidizi, Angela Shija amesema watoto hao wenye umri kati ya miaka 9 na 13 walikamatwa Januanri 30,mwaka 2018 wilayani Manyoni.
Amesema walikuwa wakitokea nchini Rwanda wakielekea nchini Zambia kuwaona wazazi wao.
“Januari 30 mwaka 2018, ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Singida ilifanikiwa kuwakamata watoto wa kike watatu raia wa Rwanda.
"Walikamatwa wilayani Manyoni mkoani Singida wakiwa kwenye basi namba T 265 BFY mali ya Kampuni ya Katagi,” amefafanua Kamishina huyo msaidizi
Kwa mujibu wa Ofisa Uhamiaji Idara ya Uhamiaji ilifanikiwa kuwakamata watoto hao kutokana na taarifa za raia wema na watoto hao wamedai wanaelekea nchini Zambia kuwaona wazazi wao.
Hata hivyo Kamishina Msaidizi huyo wa Jeshi la Uhamiaji limeweka bayana kuwa Idara ya Uhamiaji mkoani Singida inaendelea na uchunguzi ili kubaini watu waliojihusisha na biashara hiyo ya usafirishaji wahamiaji haramu.
Aidha Kaimu Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Singida ametoa mwito kwa wananchi kujenga utamaduni wa kutoa taarifa kwenye ofisi zao au kwenye vituo vya polisi vilivyo karibu mara wanapowaona watu wasiowafahamu.
Amefafanua kuwa taarifa hizo zitaisaisi Uhamiaji kufanyia kazi za kubaini matukio ya watu wa aina hiyo na kuwachukulia hatua za kisheria.
Amesisitiza baada ya uchunguzi kukamilika na kuwabaini waliohusika katika biashara hiyo ya kuwasafirisha,na kwa sababu wana umri chini ya miaka 18,watoto hao watarudishwa nyumbani kwa wazazi wao nchini Rwanda.
Watoto wa kike watatu raia wa Rwanda wenye umri chini ya miaka 18 kwa tuhuma za kuingia nchini kinyume cha sheria wakiwa kwenye ofisi za idara hiyo Mkoa Singida
Baadhi ya Maafisa Uhamiaji waliopo katika Ofisi za Mkoa wa Singida (Picha zote Na Jumbe Ismailly)
No comments:
Post a Comment