HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, February 17, 2018

UBALOZI WA KUWAIT, TAASISI YA DORIS MOLLEL WAKABIDHI MSAADA WA VIFAA TIBA VYA KUSAIDIA WATOTO NJITI KWA HOSPITALI ZA MAFIA NA WETE

Muanzilishi wa Taasisi ya Doris Mollel na Balozi wa Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (Njiti), Doris Mollel (kulia) akikabidhi Mashine maalum ya kumpa joto Mtoto anayezaliwa kabla ya wakati (Njiti) kwa Mkuu wa Kitengo cha Huduma wa Wizara ya Afya Zanzibar (Pemba), Dkt. Yussuf Hamad Iddi (kushoto) katika hafla fupi ya makabidhiano ya vifaa tiba mbalimbali vilivyotolewa kwa msaada wa Ubalozi wa Kuwait nchini, iliyofanyika kwenye Hospitali ya Wete, Kisiwani Pemba, Zanzibar Februari 16, 2018. wengine pichani ni Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Wete, Sabra Salim Suleiman (wa pili kushoto) pamoja na Muwakilishi wa Taasisi ya Doris Mollel kwa upande wa Zanzibar, Warda Walid (wa pili kulia). 
Uongozi wa Taasisi ya Doris Mollel ulioongozwa na Muanzilishi wa Taasisi hiyo na Balozi wa Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (Njiti), Doris Mollel (wa pili kulia walioketi) na Muwakilishi wa Taasisi hiyo kwa upande wa Zanzibar, Warda Walid (kulia walioketi) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Madaktari wa Hospitali ya Wete, Kisiwani Pemba, Zanzibar Februari 16, 2018, baada ya kukabidhi vifaa tiba mbalimbali vilivyotolewa kwa msaada wa Ubalozi wa Kuwait nchini.
Mkuu wa Kitengo cha Huduma wa Wizara ya Afya Zanzibar (Pemba), Dkt. Yussuf Hamad Iddi (kushoto) akizungumza jambo na uongozi wa Taasisi ya Doris Mollel ulioongozwa na Muanzilishi wa Taasisi hiyo na Balozi wa Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (Njiti), Doris Mollel(kulia) aliyeambayana na Muwakilishi wa Taasisi hiyo kwa upande wa Zanzibar, Warda Walid (wa pili kulia) wakati walipotembelea Hospitali ya Wete, Kisiwani Pemba, Zanzibar Februari 16, 2018. Katikati ni Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Wete, Sabra Salim Suleiman.
Muanzilishi wa Taasisi ya Doris Mollel na Balozi wa Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (Njiti), Doris Mollel (kushoto) akipokea taarifa fupi ya Hospitali hiyo, kutoka kwa Mkuu wa Wadi ya Wazazi Hospitali ya Wete, Bikombo Abdalla Mastur. Katikati ni Muwakilishi wa Taasisi hiyo kwa upande wa Zanzibar, Warda Walid.
Muanzilishi wa Taasisi ya Doris Mollel na Balozi wa Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (Njiti), Doris Mollel (kulia) akiwaeleza jambo wakinamama waliojigungua katika Wadi ya Wazazi juu ya swala la Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (Njiti).
 Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mafia, Zubeir Mzige (wa tatu kulia) akipokea kutoka kwa Muanzilishi wa Taasisi ya Doris Mollel na Balozi wa Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (Njiti), Doris Mollel (kushoto) sehemu ya vifaa tiba mbalimbali vya kusaidia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati, vilivyotolewa kwa msaada wa Ubalozi wa Kuwait nchini, kwenye Hospitali ya Wilaya ya Mafia, mwanzoni mwa wiki. makabidhiani hayo yalikuwa ni ya awali kabla ya kuelekea Hospitali ya Wete, Pemba.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad