HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, February 2, 2018

MAKAMU WA RAIS AWAPA POLE FAMILIA YA RUBANI WA SERIKALI KAPTENI BOMANI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo amehudhuria msiba wa Rubani wa Ndege za Serikali, Marehemu Kapteni Dominic Bomani aliyefariki jana kwa ajali ya ndege kwenye uwanja wa ndege wa Abeid Amani Karume .
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisaini kitabu cha kumbukumbu cha maombelezo ya Rubani wa Ndege za Serikali Marehemu Kapteni Dominic Bomani nyumbani kwa marehemu Kinyerezi Kanisani. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimpa pole Rosemary Bomani mjane wa aliyekuwa Rubani wa Ndege za Serikali Marehemu Kapteni Dominic Bomani nyumbani kwa marehemu Kinyerezi Kanisani. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
 akamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Rosemary Bomani mjane wa aliyekuwa Rubani wa Ndege za Serikali Marehemu Kapteni Dominic Bomani, wengine pichani ni mtoto wa marehemu Joanitha Bomani (kulia) na Dada wa marehemu Stella Bomani(kushoto) wakati alipoenda kuwapa pole nyumbani kwa marehemu Kinyerezi Kanisani. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad