HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, February 3, 2018

RAIS DK.MAGUFULI AWATUNUKU KAMISHENI MAOFISA WAPYA 192 JWTZ,WAMO PIA WA NCHI MARAFIKI

 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwatunuku Kamisheni Maafisa wapya 192 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania pamoja na Maafisa kadhaa kutoka nchi marafiki katika Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam.
  Mafisa wapya wa Jeshi la Ulinzi wakivalishana vyeo mara baada ya Kutunukiwa Kamisheni na Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Maafisa wapya wa Jeshi la Ulinzi wakila Kiapo cha Utii kwa Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika viwanja vya Ikulu mara baada ya kutunukiwa Kamisheni.
 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua gwaride la Maafisa wapya wa Jeshi la Ulinzi pamoja na baadhi kutoka nchi marafiki kabla ya kuwatunuku Kamisheni katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini (CDF) Jenerali Venance Mabeyo, Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi cha Monduli (TMA) Meja Jenerali Paul Peter Masao katika picha ya pamoja  na Maafisa wapya wa Jeshi la Ulinzi pamoja na baadhi kutoka nchi marafiki mara baada ya kuwatunuku Kamisheni.
 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipiga ngoma wakati Bendi ya Jeshi la Ulinzi ilipokuwa ikitoa burudani katika viwanja vya Ikulu mara baada ya kuisha kwa shughuli za Kutunuku Kamisheni.
 Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akielekea kutunuku Kamisheni katika Viwanja vya Ikulu
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipigiwa wimbo wa Taifa kabla ya kutunuku Kamisheni kwa maafisa wapya wapatao 192 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi pamoja na baadhi kutoka nchi marafiki. PICHA NA IKULU

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad