HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, January 25, 2018

KATIBU MKUU MAMBO YA NDANI YA NCHI AKAGUA UJENZI WA NYUMBA ZA ASKARI MAGEREZA UKONGA, JIJINI DAR ES SALAAM

 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Mstaafu, Projest Rwegasira akimsalimia Kaimu Meneja wa Mkoa wa Dar es Salaam, Wakala wa Majengo nchini (TBA-B), Manasseh Slekelaghe (Kushoto), mara baada ya Katibu Mkuu huyo kumaliza ziara yake ya ukaguzi wa ujenzi wa nyumba za askari Magereza, zilizopo Ukonga, jijini Dar es Salaam leo.  Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Mstaafu, Projest Rwegasira (wapili kushoto) akimsikiliza Mratibu wa Mradi wa Ujenzi wa Nyumba za Askari Magereza, Mhandisi Khadija Salum, alipokua anamuonyesha Katibu Mkuu huyo maeneo mbalimbali ya ujenzi wa nyumba hizo zilizopo Ukonga, jijini Dar es Salaam. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Moja ya jengo la Makazi ya Askari Magereza likionekana hatua iliyofikia. Nyumba hizo zilizopo Ukonga jijini Dar es Salaam, zinajengwa na Wakala wa Majengo nchini (TBA-B) na kusimamiwa na Jeshi la Magereza nchini. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Mstaafu, Projest Rwegasira akiwafafanulia jambo wajenzi wa Nyumba za Askari Magereza zilizopo Ukonga jijini Dar es Salaam, ambao ni Wakala wa Majengo nchini (TBA-B).  Kushoto (meza kuu) ni Kaimu Meneja wa Mkoa wa Dar es Salaam (TBA-B), Manasseh Slekelaghe, anaefuata ni Mratibu wa Mradi wa Ujenzi wa Nyumba hizo, Mhandisi Khadija Salum, na kushoto ni Mhandisi wa Mradi huo, Peter Kikwati. Kulia ni Msimamizi wa Mradi wa huo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Magereza, Cosmas Mtambala. Katibu Mkuu alizikagua nyumba hizo leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Mstaafu, Projest Rwegasira akiwafafanulia jambo wajenzi wa Nyumba za Askari Magereza zilizopo Ukonga jijini Dar es Salaam, ambao ni Wakala wa Majengo nchini (TBA-B), pamoja na wasimamizi wa mradi huo ambao ni Maafisa wa Jeshi la Magereza.  Kushoto (meza kuu) ni Kaimu Meneja wa Mkoa wa Dar es Salaam (TBA-B), Manasseh Slekelaghe. Katibu Mkuu alizikagua nyumba hizo leo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad