HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, January 11, 2018

DKT. TULIA AKABIDHI TV SITA TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE

 Naibu Spika wa Bunge Mhe.  Dkt.  Tulia Ackson akimkabidhi Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Fedha Agnes Kuhenga Televisheni moja kati ya nne zilizotolewa na Taasisi ya Tulia (Tulia Trust Fund) kwa ajili ya watoto wanaotibiwa katika Taasisi hiyo. Jumla ya TV sita zimetolewa na Tulia Trust ambazo zimefungwa  katika wodi na kliniki za watoto.
  Kaimu Mkurugenzi wa Tiba Shirikishi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambaye pia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo Delila Kimambo akimweleza  Naibu Spika wa Bunge Mhe. Dkt.  Tulia Ackson maendeleo ya afya za pacha walioungana Maria na Consolata waliolazwa  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya Matibabu.
 Naibu Spika wa Bunge Mhe. Dkt.  Tulia Ackson akiwajulia hali pacha walioungana Maria na Consolata waliolazwa  katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)kwa ajili ya Matibabu.
 Naibu Spika wa Bunge Mhe. Dkt. Tulia Ackson akiwajulia hali watoto waliolazwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya matibabu.  Mhe. Dkt. Tulia kupitia Taasisi ya Tulia (Tulia Trust Fund) ametoa TV sita kwa JKCI ambazo zimefungwa  katika wodi na kliniki za watoto. Picha na JKCI 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad