HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, December 21, 2017

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YAZINDUA VYOMBO VYA KUSIMAMIA BIASHARA YA UTALII NCHINI

 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akizungumza na Wajumbe na Wenyeviti  kwenye hafla ya uzinduzi wa vyombo vya kusimamia Biashara ya Utalii nchini (TTLB) vikijumuisha  Bodi ya Leseni ya Biashara ya Utalii, Kamati ya ushauri ya Utalii na Mamlaka ya Rufaa ya Utalii zilizonduliwa leo jijini Dar es Salaam. ( Picha na Lusungu Helela- MNRT)
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga ( wa kwanza kulia) akizungumza na  Mwenyekiti wa Bodi ya Leseni za Biashara za Utalii  Saleh Pamba ( wa pili kushoto)   katika hafla ya uzinduzi wa  vyombo vya kusimamia Biashara ya Utalii (TTLB) nchini iliyofanyika  leo jijini Dar es Salaam. Wengine ni Naibu Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii, Alovce Nzuki,     ( wa tatu kushoto) Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Deograsias Mdamu, ( wa pili kulia)  Mjumbe wa Bodi ya TTLB, Michael Kamba  (wa  kwanza kushoto) ( Picha na Lusungu Helela- MNRT) 
 Mwenyekiti wa Bodi ya Leseni za Biashara za Utalii  Saleh Pamba ( wa pili kushoto) akizungumza na  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga ( wa kwanza kulia)   katika hafla ya uzinduzi wa  vyombo vya kusimamia Biashara ya Utalii (TTLB) nchini iliyofanyika  leo jijini Dar es Salaam. Wengine ni Naibu Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii, Alovce Nzuki, ( wa tatu kushoto) Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Deograsias Mdamu, ( wa pili kulia)  Mjumbe wa Bodi ya TTLB, Michael Kamba  (wa  kwanza kushoto) ( Picha na Lusungu Helela- MNRT)
 Mwenyekiti wa Mamlaka ya Rufaa ya Utalii, Balozi Mwanaidi Maajar akizungumza na Wajumbe na Wenyeviti  kwenye hafla ya uzinduzi wa vyombo vya kusimamia Biashara ya Utalii nchini (TTLB)  vikijumuisha  Bodi ya Leseni ya Biashara ya Utalii, Kamati ya ushauri ya Utalii na Mamlaka ya Rufaa ya Utalii zilizonduliwa leo jijini Dar es Salaam. ( Picha na Lusungu Helela- MNRT)
 Mwenyekiti wa Kamati ya  Ushauri ya Utalii, Prof. Wineaster Anderson akitoa neno la shukrani kwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekeiti kwenye kamati hiyo kwenye hafla ya uzinduzi wa vyombo vya kusimamia Biashara ya Utalii nchini (TTLB) vikijumuisha  Bodi ya Leseni ya Biashara ya Utalii, Kamati ya ushauri ya Utalii na Mamlaka ya Rufaa ya Utalii zilizonduliwa leo jijini Dar es Salaam. ( Picha na Lusungu Helela- MNRT
 Baadhi ya Wajumbe na Wenyeviti waliochaguliwa wakiwa   katika hafla ya uzinduzi wa vyombo vya kusimamia Biashara ya Utalii nchini (TTLB) vikijumuisha ni  Bodi ya Leseni ya Biashara ya Utalii, Kamati ya ushauri ya Utalii na Mamlaka ya Rufaa ya Utalii zilizonduliwa leo jijini Dar es Salaam. ( Picha na Lusungu Helela- MNRT)
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na  Wajumbe na Wenyeviti  kwenye hafla ya uzinduzi wa vyombo vya kusimamia Biashara ya Utalii nchini (TTLB) vikijumuisha   Bodi ya Leseni ya Biashara ya Utalii, Kamati ya ushauri ya Utalii na Mamlaka ya Rufaa ya Utalii zilizonduliwa leo jijini Dar es Salaam. ( Picha na Lusungu Helela- MNRT)

Wizara ya Maliasili na Utalii  imefanya uzinduzi wa vyombo vya kusimamia biashara ya utalii nchini katika Chuo cha Taifa cha  Utalii kilichopo jijini Dar es salaam, ambapo vyombo hivyo vimejumuisha kamati ya ushauri,Mamlaka ya rufaa pamoja na Bodi ya mamlaka ya leseni.

Akiongea leo katika uzinduzi huo Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japheth Hasunga amewapongeza wanakamati wote waliochaguliwa na kusema kuwa anaamini kuwa watafanya kazi kwa umoja na ushirikiano ili kuhakikisha kuwa sekta ya utalii inapiga hatua kusonga mbele.

Pia, Naibu  Waziri Hasunga amesisitiza kuwa vyombo hivyo vya kusimamia biashara ni vyombo muhimu sana katika kuendeleza sekta ya utalii na wajumbe wa vyombo hivyo ni muhimu kwa kusimamia sekta ya utalii nchini.

"Ni vyombo muhimu sana katika kuendeleza sekta ya utalii na wajumbe wa vyombo hivi ni muhimu sana kwa kusimamia sekta ya utalii hapa nchini" amesema Hasunga.

Aidha, Hasunga ameiomba Bodi ya Leseni ya Utalii iliyochaguliwa kufanya kazi katika misingi mikuu mitatu ya utawala bora ambayo ni Uhuru, uwazi, usawa na uzalendo ili kuepukana na migongano na kutokuelewana nyakati za kazi.

"Nawaomba mfanye kazi katika misingi ya utawala bora Uhuru, usawa, Haki na uzalendo"amesema Hasunga.

Katika hatua nyingiune, Naibu Waziri Hasunga amesema  kuwa sekta ya utalii ni sekta  inayochangia  kiasi kikubwa pato la Taifa  pia inasaidia upatikanaji wa fedha za kigeni kwa urahisi, hivyo amewaomba watanzania kuwa wazalendo kwa kuhamasisha uhifadhi wa mazingira pamoja na utamaduni wa mtanzania ili vivutio vizidi kuwepo kwani wasipotunza mazingira utalii hautaendelea kuwepo.

Pia amesema kuwa japo Tanzania ina vivutio vingi vya utalii bado mapato ni madogo ukilinganisha na vivutio vilivyopo hivyo ameeleza mikakati ya serikali kuwa imepanga kufikia watalii milioni mbili mpaka ifikapo mwaka 2020 ambapo jukumu hilo ni la kila Mtanzania.

"Mapato ni madogo ukilinganisha na vivutio vilivyopo na serikali tumepanga kufikia watalii milioni mbili ifikapo mwaka 2020 ni jukumu letu sote kuhakikisha tunafikia idadi hiyo. amesema Hasunga.

Pia ameisistiza Bodi ya leseni ya utalii kuhakikisha leseni za biashara zinatolewa kwa wakati na kwa kuzingatia kanuni, taratibu na sheria zilizopo.

"Mhakikishe leseni zinatolewa kwa wakati sahihi bila kucheleweshwa kwa kuzingatia kanuni, taratibu na sheria kama inavyosema"amesema Hasunga.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad