HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, December 25, 2017

WASHINDI WA DROO YA PILI MLIMANI CITY WAPATIKANA.

Na Mwandishi Wetu.
WASHINDI 20 wa promosheni ya Mlimani City Shoping Fest wamepatika mara baada ya kucheza droo iliyofanyika mwishoni mwa wiki Mlimani City jijini Dar es Salaam ambao ni Grace Mushi,Samson K. Samson,Grace Hoka, Mnyamani, Mushi Kimaro, Judith Shayo, Erick Msumati, Gwamaka Hezron, Ally Nyaga, Amani Sepetu, Masood Wanani, Jonathan Nkya, Hellen Mngutu, Omary Khary, Linda Bahati, Agrum Maringo, Saidi Kheri, Paul Charles, Beatrice Kaswaga na Suzan Said.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mratibu wa Kampeni hiyo, Neema Utouh alisema mpaka sasa jumla ya washindi 40 wamepatikana tangu Kampeni hiyo izinduliwe rasmi na tayari zawadi zao za vocha ya kufanya manunuzi yenye thamani ya Shilingi 100,000 kila mmoja wameshapatiwa.
Alisema Neema, ni nafasi yakow ewe ambaye hujaja kufanya manunuzi mlimani City karibia fanya manunuzi ya shilingi laki moja au zaidi utapewa kuponi ambayo itakuwezesha kuingia moja kwa moja kwenye droo ya ushindani.
Hii ni wiki ya pili taku promosheni hii izinduliwe na bado wiki tatu ambapo mwisho kabisa kutakuwa na droo kubwa ambayo mshindi mmoja atajishindia vocha yenye thamani ya shilingi 10,000 000 ambayo itamuwezesha kufanya manunuzi duka lolote ndani ya Mlimani City pamoja na washindi watano watakaojishindia vocha yenye thamani ya shilingi milioni moja kila mmoja.
Mwisho Neema alitoa wito kwa wateja wa mlimani City na watu wote kujitokeza kwa wingi kuja kufanya manunuzi Mlimani City katika kipindi hiki cha siku kuu ya Chrismass na Mwaka mpya ili kupata fursa ya kushiriki katika shindano la promosheni ya “Mlimani City Shopping Fest”.

AKatika kusherehekea Sikukuu za X-Mas na Mwaka Mpya, uongozi wa Mlimani City kwa kushirikiana na wafanyabiashara wenye maduka ndani yake umetangaza ofa maalumu kwa wateja  wake watakaofanya manunuzi katika msimu huu wa sikukuu.
Ofa hiyo inatoa fursa ya kujishindia zawadi mbalimbali ambazo zimegawanywa kwa makundi matano ambapo kila wiki washindi 20 watajishindia vocha yenye thamani ya kufanya shoping kwa vitu vya thamani ya Shilingi 100,000 lakini pia watakuwa mwameingia moja kwa moja kwenye droo kubwa ya mwisho ambayo mshindi wa kwanza atajishindia vocha ya manunuzi ya bidhaa za nyumbani yenye thamani ya Shilingi Milioni 10, na mshindi 5 watajinyakulia vocha yenye thamani ya shilingi milioni 1, kila mmoja.  

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Meneja mkuu wa Mlimani City Ndugu Pastory Mrosso alisema kuwa washindi wa kila wiki watafanya manunuzi katika duka lolote ndani ya Mlimani City kwa kutumia vocha zao.
Promosheni hii maalumu imeanza Desemba 15 na inatarajia kufikia mwisho Januari 14, 2018, ambapo droo kubwa ya kupata mshindi wa kwanza wa Vocha yenye thamani ya Shilingi milioni 10.
Meneja huyo aliwaomba watanzania kuendelea kufanya manunuzi yao katika maduka ya Mlimani City, kutokana na kuwajali wateja wake na kutoa huduma zinazokwenda na wakati na hasa katika kipindi hiki cha X-Mas na Mwaka Mpya.
 Coordinator/Mratibu wa promosheni ya fanya manunuzi mlimani City na ushinde(Grand Shopping fest), Neema Utouh akichanganya kuponi ili kupata washindi 20 wa droo ya pili wa vocha ya thamani ya Shilingi 100,000 kila mmoja ya kufanya manunuzi tena katika duka lolote ndani ya Mlimani City iliyofanyika mwishoni mwa wiki Mlimani City Dar es Salaam.Wengine ni mabalozi wa Promosheni hiyo.
 Coordinator/Mratibu wa promosheni ya fanya manunuzi mlimani City na ushinde(Grand Shopping fest), Neema Utouh akifungua kuponi ya msindi wa kwanza wa droo ya pili wa vocha ya thamani ya Shilingi 100,000 ya kufanya manunuzi tena katika duka lolote ndani ya Mlimani City iliyofanyika mwishoni mwa wiki Mlimani City Dar es Salaam.Wengine ni mabalozi wa Promosheni hiyo.
Coordinator/Mratibu wa promosheni ya fanya manunuzi mlimani City na ushinde(Grand Shopping fest), Neema Utouh(kushoto) akimkabidhi vocha ya thamani ya Shilingi 100,000, Grace Mushi mara baada ya kuibuka mshindi katika droo ya pili ya promosheni ya fanya manunuzi Mlimani City na ushinde(Mlimani City Grand Shopping Fest) iliyofanyika Mlimani City mwishoni mwa wiki.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad