Wananchi wote wa Mkoa wa Simiyu wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika zoezi la
uandikishaji Vitambulisho vya taifa (NIDA) linaloendelea mkaoni humo.
Wito huo umetolewa na Afisa Tawala Wilaya ya Bariadi ndg. Rutaihnwa Albert ambaye
pia amewataka watendaji wa Kata pamoja na wasimamizi kuweka utaratibu mzuri wa
wananchi Kusajiliwa pindi wanapofika kwenye vituo vya Usajili.
Aidha wananchi wametakiwa kufika kwenye vituo vya usajili wakiwa na nakala
(photocopy) ya viambatisho vyao muhimu vinavyo hitajika kuwasajili ambavyo ni Cheti
cha Kuzaliwa, Pasi ya Kusafiria (Passport), Vyeti vya Elimu ya Msingi na Sekondari,
Leseni ya Udereva, Kitambulisho cha Bima ya Afya, Nambari ya Mlipa Kodi (TIN No.) na
Kitambulisho cha Mpiga kura pamoja na kuzingatia taratibu za usajili pindi wanapokuwa
kwenye vituo.
Zoezi la Usajili Vitambulisho vya Taifa kwa sasa linaendelea katika mikao 15(kumi na
tano ya Tanzania) ambapo kwa mkoa wa Simiyu zoezi linaendelea kwa Kata za
Senani, Mwamanenge na Ipililo.
Wananchi mkoani Simiyu wakiwa katika foleni kusubiri kuchukuliwa alama
za kibaiolojia baada ya kukamilisha zoezi la kujaza fomu za maombi ya
Kitambulisho cha Taifa.
Mwananchi wa kijiji cha Ditima akiwa katika meza ya Mwenyekiti wa Mtaa
akisubiri fomu yake kukaguliwa na kusainiwa ili aweze kwenda kuchukuliwa
alama za kibaiolojia zinazojumuisha kupigwa picha, kuweka saini na
kuchukuliwa alama za viganja(finger print).
Mmoja wa wananchi akijaza fomu ya maombi ya Kitambulisho cha Taifa
wakati Mwenyekiti wa mtaa wa Ditima akichambua fomu walizojaza
wananchi na kuwapatia ili wakashiriki katika hatua ya pili ya Usajili ikiwa ni
kuchukuliwa alama za kibaiolojia.
No comments:
Post a Comment