HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, December 4, 2017

WABUNGE TUMIENI MICHEZO KUIMARISHA USHIRIKIANO WA EAC-MAJALIWA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wachezaji wa timu ya Bunge la Tanzania muda mfupi kabla ya kuanza kwa mechi dhidi ya timu ya Bunge ya Burundi alipofungua mashindano ya mabunge ya nchi za Afrika Mashariki kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam leo Desemba 4, 2017. 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wachezaji wa timu ya Bunge la Burundi muda mfupi kabla ya kuanza kwa mechi dhidi ya timu ya Bunge ya Tanzania alipofungua mashindano ya mabunge ya nchi za Afrika Mashariki kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam leo Desemba 4, 2017. PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka wabunge wanaoshiriki mashindano ya Mabunge ya Jumuiya ya Afrika Mashariki wayatumie kuimarisha ushirikiano.
Ametoa kauli hiyo leo (Jumatatu, Desemba 4, 2017) wakati akifungua mechi ya mpira wa miguu iliyozikutanisha timu za Tanzania na Burundi kwenye Uwanja wa Taifa.

Mashindano hayo ya Nane ya Mabunge ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yalifunguliwa jana (Jumapili, Desemba 3, 2017) na Spika wa Bunge Job Ndugai

Waziri Mkuu amesema nchi zote zinashiriki mashindano hayo ni  ndugu hivyo ni vema wakayatumia katika kuimarisha ushirikiano wa Mabunge ya Jumuiya hiyo.

Pia Waziri Mkuu amewataka wachezaji hao kuhakikisha kucheza mpira mzuri na wazingatie viwango vya Shirikisho la Soka Duniani (FIFA).

Hata hivyo Waziri Mkuu amesema katika mashindano hayo kila timu inahitaji kupata ushindi, hivyo amewataka wanatumie vizuri ujuzi wao ili waibuke na ushindi.

Katika ufunguzi huo Waziri Mkuu aliambatana na Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Dkt. Tulia Akson, Katibu wa Bunge la Tanzania Stephen Kagaigai.

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt.  Harrison Mwakyembe.

Katika mashindano hayo timu ya Tanzania imeibuka kidedea baada ya kushinda magoli matatu na Burundi ilipata magoli mawili.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
JUMATATU, DESEMBA 4, 2017.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad