Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa
inavitangazia Vyama vya Siasa na umma kwa ujumla kuwa kikao na Semina ya Baraza
la Vyama vya Siasa vilivyokuwa vifanyike siku ya tarehe 21 na 22 Disemba 2017,
Jijini Dar es Salaam vimeahirishwa hadi hapo tarehe nyingine itakapopangwa.
Kikao hicho kimeahirishwa kwa ajili ya kutoa
fursa kwa Vyama vya Siasa na wadau wa Vyama vya Siasa kushiriki katika shughuli za uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika 13 Januari
2018. Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote
utakaojitokeza kutokana na mabadiliko hayo.
Jacqueline Kilama
Kny: MSAJILI
WA VYAMA VYA SIASA
19 Disemba, 2017
No comments:
Post a Comment