HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, December 27, 2017

RC INJINIA NDIKILO ATAKA KILUVYA UNITED WAIFUNGE RUVU SHOOTING JUMAMOSI

MKUU wa Mkoa wa Pwani Inginia Everist Ndikilo leo ametoa hamasa kwa kuichangia  timu ya Kiluvya United  kiasi cha  Sh. Mil.2.2 ikiwa kwa ajili ya kuweka kambi  kuelekea mechi yao na Ruvu Shooting  itakayopigwa Desemba 30 mwaka huu katika uwanja wa Filbert Bayi uliopo Mkuza  Kibaha Mkoani Pwani ambapo timu hizo zitakutana katika kuwania kucheza Ligi Kuu Bara msimu ujao.

Injinia Ndikilo amewataka wachezaji wa timu ya Kiluvya United kucheza kufa na kupona ili iweze kupanda daraja na kuleta sifa katika mkoa wa Pwani

Injia ndikilo amesema hayo alipozungumza na wachezaji hao ofisini kwake  Kibaha Mkoani Pwani huku akiwasisitiza kuibuka na ushindi kwenye mechi hiyo.

Katika  hamasa  hiyo Mheshimiwa  Ndikilo ametoa Sh. Mil. 2.2  kwa timu hiyo  inayocheza Ligi  Daraja la Kwanza ambayo inawania kupanda  nankuweza kuingia kwenye  mzunguko wa Ligi Kuu Bara katika msimu ujao.

Kiluvya United itashuka dimbani  kukipiga na timu ya Ruvu Shooting  Desemba  30 mwaka huu katika uwanja wa Filbert Bayi  uliopo maeneo ya Mkuza Kibaha Mkoani Pwani.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad