Katika kuadhimisha
Miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania Bara tarehe
9 Disemba, 2017 Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa
kutumia madaraka aliyopewa chini ya Ibara ya 45(1)(d) ya Katiba ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania ametoa msamaha kwa wafungwa wafuatao:-
(i)
Wafungwa wote
wapunguziwe moja ya sita (1/6) ya vifungo vyao zaidi ya
punguzo la kawaida la moja ya tatu (1/3)
linalotolewa chini ya Kifungu 49(1) cha Sheria ya Magereza Sura ya 58,
isipokuwa wafungwa walioorodheshwa katika Ibara ya 2(i – xxi).
(ii)
Wafungwa wagonjwa wenye
magonjwa kama UKIMWI, Kifua kikuu (TB) na Saratani (Cancer) ambao wako kwenye “terminal stage”. Wafungwa hawa
wathibitishwe na Jopo la Waganga chini ya Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga Mkuu wa Wilaya.
(iii)
Wafungwa wazee wenye
umri wa miaka sabini (70) au zaidi. Umri
huo uthibitishwe na Jopo la Waganga chini ya Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa Mkoa/Mganga Mkuu wa Wilaya.
(iv)
Wafungwa wa kike
walioingia na mimba gerezani, pamoja na wale walioingia na watoto wanaonyonya
na wasionyonya.
(v)
Wafungwa wenye ulemavu
wa mwili na akili (Physical disability
and mental disability). Ulemavu huo uthibitishwe na Jopo la Waganga chini
ya Uenyekiti wa Mganga Mkuu wa
Mkoa/Mganga Mkuu wa Wilaya.
2. Aidha,
Msamaha wa Mheshimiwa Rais hautawahusu wafungwa wafuatao:-
(i)
Wafungwa waliohukumiwa
adhabu ya kunyongwa au kwa makosa ya kujaribu kuua (attempt to murder).
(ii)
Wafungwa waliohukumiwa
adhabu ya kunyongwa na adhabu hiyo kubadilishwa kuwa kifungo cha maisha au
kifungo gerezani.
(iii)
Wafungwa waliohukumiwa
kifungo cha maisha gerezani.
(iv)
Wafungwa wanaotumikia
kifungo kwa makosa ya kujihusisha na usafirishaji na matumizi ya madawa ya
kulevya kama vile cocaine, heroin,
bhangi n.k.
(v)
Wafungwa wanaotumikia
kifungo kwa makosa ya kujihusisha na uombaji na upokeaji au utoaji rushwa.
(vi)
Wafungwa wanaotumikia
kifungo kwa makosa ya unyang’anyi na unyang’anyi wa kutumia silaha au kujaribu kutenda
makosa hayo (robbery with violence,
armed robbery and attempted robbery).
(vii)
Wafungwa wanaotumikia
kifungo kwa makosa ya kupatikana na silaha, risasi au milipuko isivyo halali (fire arms, ammunitions and explosives).
(viii)
Wafungwa wanaotumikia
kifungo kwa makosa ya shambulio la aibu, kunajisi, kubaka na kulawiti, ukatili
kwa watoto au kujaribu kutenda makosa hayo.
(ix)
Wafungwa waliopatikana
na hatia na kuhukumiwa kifungo kwa kosa la kuwapa mimba wanafunzi wa Shule za
Msingi na Shule za Sekondari na ambao walitenda kosa hilo wakiwa na umri wa
miaka kumi na nane (18) na kuendelea.
(x)
Wafungwa wanaotumikia
kifungo kwa makosa ya wizi wa magari na pikipiki, uharibifu wa miundombinu au
kujaribu kutenda makosa hayo.
(xi)
Wafungwa wanaotumikia
kifungo chini ya Sheria ya Bodi ya Parole (Act. No. 25/1994) na Sheria ya
Huduma kwa Jamii (Act. No. 6/2002).
(xii)
Wafungwa waliopatikana
na hatia na kuhukumiwa kifungo kwa makosa ya kutumia vibaya madaraka yao na
kuhujumu uchumi.
(xiii)
Wafungwa waliowahi
kupunguziwa kifungo na Msamaha wa Mhe. Rais na bado wangali wanaendelea
kutumikia sehemu ya kifungo kilichobaki.
(xiv)
Wafungwa waliopatikana
na hatia na kuhukumiwa kwa kosa la kuzuia watoto kupata masomo.
(xv)
Wafungwa waliopatikana
na hatia na kuhukumiwa kwa kosa la utekaji wa watoto, kupoka na kufanya
biashara ya binadamu (Human Trafficking).
(xvi)
Wafungwa waliopatikana
na hatia na kuhukumiwa kwa kosa la kukutwa na viungo vya binadamu.
(xvii)
Wafungwa wanaotumikia
vifungo kwa makosa ya kujihusisha kwa namna yoyote ile na nyara za Serikali na
ujangili (poachers).
(xviii)
Wafungwa wanaotumikia
vifungo kwa makosa ya wizi/ubadhirifu wa fedha za Serikali.
(xix)
Wafungwa wanaotumikia vifungo kwa makosa
ya kutoroka au kujaribu kutoroka chini ya ulinzi halali.
(xx)
Wafungwa walioingia gerezani baada ya
tarehe 30/10/2017.
(xxi)
Wafungwa waliowahi kufungwa gerezani.
3. Wafungwa 8,157 watafaidika na msamaha huu ambapo 1,828 wataachiliwa huru tarehe 9
Disemba, 2017 na 6,329 watabaki
gerezani kumalizia sehemu ya kifungo kilichobaki baada ya kupewa msamaha huu. Ni
mategemeo ya Serikali kwamba watarejea tena katika jamii kushirikiana na wenzao
katika ujenzi wa Taifa na kwamba watajiepusha kutenda makosa ili wasirejee tena
gerezani.
Aidha Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa mujibu wa Ibara ya
45(1) (d) ya Katiba ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania inampa Mamlaka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
kufuta adhabu yote au sehemu ya adhabu yoyote aliyopewa mtu yeyote kwa
ajili ya kosa lolote au kufuta adhabu yote.
Kwa
kutumia Mamlaka aliyo nayo amewasamehe wafungwa wengine 63
kati yao wafungwa 61 ni wale waliokuwa wamehukumiwa kunyongwa, waliokuwa
na umri mkubwa na waliokaa gerezani muda mrefu. Na pia
amewasamehe wafungwa wengine wawili waliokuwa wakitumikia kifungo cha maisha
ambao ni Nguza Viking(BABU SEA) na
Johnson Nguza. Hivyo kwa ujumla amewasamehe wafungwa 8220.
imetolewa na
Meja Jenerali Projest Rwegasira (Mstaafu)
KATIBU MKUU
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
09/12/2017
No comments:
Post a Comment