HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, December 9, 2017

BABU SEYA, PAPII KOCHA WATOKA GEREZANI JIONI HII

Mwanamuziki Nguza Viking (Babu Seya) pamoja na Mwanaye Papii Kocha wakipunga mikono muda huu baada ya kutoka katika Gereza la Ukonga jijini Dar es salaam wakokuwa wanatumikia kifungo cha maisha na sasa wameachiwa huru kwa msamaha wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli alioutoa leo huko Mjini Dodoma kulikofanyika Maadhimisho ya miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania Bara. Babu Seya na Mwanawe ni sehemu ya wafungwa 8157 walipata msamaha wa Rais.
Babu Seya akitoka gerezani jioni hii.
Baadhi ya mashabiki wa wanamuzi wakiwa nje ya gereza la Ukonga Dar es Salaam wakimsubiri mwanamuziki Nguza Viking na mtoto wake Papi Kocha waliokuwa wanatumikia kifungo cha maisha jela na sasa wamepata msamaha. Picha na Said Mwinshehe, Globu ya Jamii.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad