HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, December 13, 2017

MKUU WA WILAYA YA TEMEKE AZINDUA JUKWAA LA WANAWAKE WILAYANI HUMO

Mkuu wa Wilaya ya Temeke
Felix Lyaniva azindua jukwaa la wanawake Kiwilaya katika viwanja vya Mwembe Yanga. Katika uzinduzi huo DC Lyaniva asisitiza wanawake kupendana,kuwa na umoja ili kujiletea maendeleo ya kweli,hata kufikia uchumi wa kati.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaniva akiwa akishuhudia wakina mama wakipiga na mabanho yenye ujumbe tofauti katika uzinduzi wa jukwaa la wanawake Wilaya ya Temeke.

Wanawake hao ambao wamejitokeza kwa wingi katika uzinduzi huo, huku sherehe hizo zikipambwa na shamrashamra za maandamano ya vikundi mbalimbali vya wanawake wajasiriamali.
Pia wanawake wajasiriamali walionesha kazi za mikono na ubunifu ufanywao na vikundi vyao.
Katika uzinduzi huo ulifanyika uchaguzi wa mwenyekiti wa jukwaa la wanawake Kiwilaya ambapo Johari Maulid Mkonde alichaguliwa rasmi kuwa mwenyekiti wa jukwaa la wanawake wilayani Temeke.
Hata hivyo wanawake wa Temeke wamepewa fursa kushiriki uchumi wa viwanda ili waweze kufika malengo ya maendeleo endelevu ya 50/50 ya dunia kufikia mwaka 2030.
Jukwa la wanawake liliundwa ili kuwawezesha wanawake kiuchumi na kuondoa pengo kubwa ambalo limejengeka duniani na kuongeza ushiriki wa wanawake katika uchumi duniani kote. Majukwaa haya yatazinduliwa katika Mikoa yote nchini na Halmashauri zote. Katika Mkoa wa Dare Es Salaam Wilaya ya Temeke ni Wilaya ya kwanza kuzindua jukwaa la wanawake.
Kauli mbiu katika uzinduzi huu ni ''Mwanamke Tumia Fursa Kushiriki Uchumi wa Viwanda''

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad