HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, December 22, 2017

MKURUGENZI MKUU WA SUMATRA ATINGA KITUO CHA UBUNGO KUANGALIA HALI YA USAFIRI KATIKA KUELEKEA SIKUKUU ZA MWISHO WA MWAKA

 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti ya  Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), Gilliard Ngewe akipata maelezo kutoka kwa Kamanda wa Usalama Barabarani Mkoa wa Kinondoni, Solomon Mwangamilo(kushoto) wakati ukaguzi wa mabasi katika kituo kikuu cha mabasi Ubungo leo jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti ya  Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), Gilliard Ngewe(kulia)  akimpa  maelezo Mkaguzi wa mabasi wa Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo, Insp. Ibrahimu Samwix(kushoto) wakati wa ukaguzi wa mabasi katika kituo kikuu cha Mabasi leo jijini Dar es Salaam.
  Mkurugenzi wa barabara wa  Sumatra, SACP Johansen Kahatano(kushoto) akimpa maelezo Mkaguzi wa mabasi wa Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo, Insp. Ibrahimu Samwix (kulia) wakati wa ukaguzi wa mabasi katika kituo kikuu cha Mabasi leo jijini Dar es Salaam.
 Kamanda wa Usalama Barabarani Mkoa wa Kinondoni, Solomon Mwangamilo(kushoto) akiangalia ukaguzi unaofanywa na Mkaguzi wa mabasi wa Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo, Insp. Ibrahimu Samwix(kulia)  leo wakati wa ukaguzi wa mabasi katika kituo kikuu cha mabasi ubungo leo jijini Dar es Salaam.
 Askari wa Usalama barabarani wa ukaguzi wa Kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo, Nuru Hussein akimpa maelekezo dereva wa basi katika kituo kikuu cha mabasi Ubungo leo jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya abiria wakiwa katika kituo kikuu cha mabasi Ubungo wakisubiri muda wa basi kuondoka katika kituo kikuu cha mabasi Ubungo leo jijini Dar es  Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad