HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, December 22, 2017

MIKOA YA KUSINI KUPATA UMEME WA UHAKIKA

 Mwenyekiti wa Bodi ya TANESCO Dkt. Alexender Kyaruzi (katikati) na wajumbe wa bodi ya Shirika hilo, wakipatiwa maelezo walipotembelea kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Mahumbika mkoani Lindi

Na Yasini Silayo
Shirika la Umeme Tanzania  TANESCO limewahakikishia Umeme wa uhakika wakazi wa Mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma kutokana na uboreshwaji mkubwa wa huduma za Uzalishaji, Usafirishaji na Usambazaji Umeme zinazoendelea katika Mikoa hiyo.
Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa TANESCO, Dkt. Alexander Kyaruzi alipofanya Ziara ya kikazi katika mikoa ya Lindi na Mtwara akiambatana na wajumbe wengine wa bodi pamoja na viongozi waandamizi wa TANESCO Makao Makuu na Kanda ya Kusini.
Akiongea na wananchi pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali Mkoani Lindi, Dkt. Kyaruzi amesema kuwa tayari TANESCO imefanya matengenezo makubwa katika mitambo ya kuzalisha umeme wa Gesi wa Megawati 18. Mtambo huo unahudumia Mikoa ya Mtwara pamoja na Baadhi ya maeneo ya Lindi kupitia laini mpya ya 132kV Mtwara-Mahumbika iliyokamilika tangu mwezi Julai mwaka huu ikijengwa na mafundi wazawa kutoka ndani ya TANESCO kupitia kampuni Tanzu yake iitwayo ETDCO.
"Mbali na hali ya umeme kuimarika hivi sasa kutokana na matengenezo ya mitambo ya Mtwara, Shirika hivi sasa linaendelea na maandalizi ya ujenzi wa miradi miwili mikubwa ya Uzalishaji Umeme wa jumla ya megawati 540 Katika Mikoa hii pamoja na kuunga mikoa ya Kusini katika Umeme wa Grid ya Taifa kwa Laini kubwa ya Msongo wa Kilovolt 400. Awamu ya kwanza ya ujenzi wa Mradii huu itakuwa kutoka Kinyerezi DSM mpaka somangafungu Lindi ambapo patajengwa mtambo wa kuzalisha umeme wa Megawati 240, mradi tayari umekwishaanza kwa kulipa fidia wananchi walioko eneo la mradi ili wapishe kupitisha laini hiyo. Awamu nyingine itaunga Somanga mpaka Mtwara ambapo kutajengwa pia mradi mkubwa wa kuzalisha umeme wa Megawat 300. Songea tayari inaunganishwa na gridi kupitia makambako na mradi unaelekea kukamilika kwa asilimia kubwa" alisema Dkt. Kyaruzi
Aliongeza kuwa kutokana na mikakati ya muda mfupi, ya kati na muda mrefu iliyowekwa na TANESCO na Serikali ya awamu ya tano kwa ujumla, matatizo ya umeme katika mikoa hiyo yatakuwa yamepatiwa ufumbuzi wa kudumu na hivyo kuchochea hamasa ya maendeo ya kiuchumi na Kijamii katika ukanda huo.
Aliongeza kuwa TANESCO inatarajia kupanua mifumo yake ya kusambaza umeme na kuiunga na mifumo ya pamoja ya nchi za Kusini mwa bara la Africa, Southern African Power pool (SAAP) kupitia Zambia pamoja na ile ya Africa Mashariki Kupitia Nchi ya Kenya. Baada ya kuunganisha mifumo
hiyo Nchi itaweza kununua na hasa kuuza ziada ya umeme kwa Nchi hizo pale itakapohitajika.
Aidha naye Mjumbe wa Bodi hyo Dkt. Lugano Wilson alisisitiza wakandarasi wa miradi ya umeme katika mkoa huo na mikoa mingine kwa ujumla kuhakikisha wanazingatia Viwango na Ubora wa kazi ili miradi hii iweze kutimiza lengo kusudiwa la kuwahudumia wananchi kwa umeme wa uhakika na kuchochea maendeo ya kiuchumi na kijamii.
"Mnapotekeleza miradi hii kwa ubora na viwango vinavyotakiwa, wananchi watapata umeme wa uhakika na kwa Upande wa TANESCO mtatupunguzia gharama za matengenezo ya mara kwa mara yatokanayo na ujenzi wa laini yenye kiwango duni" alisema Dkt. Lugano
Kwa upande wa wananchi wa maeneo hayo walionesha kufarijika na kupata shauku kubwa ya kuunganishwa na kuboreshewa huduma za umeme ambapo mwananchi mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja la Shabani alisema kuwa "Licha ya changamoto za Umeme tulizokuwa nazo kipindi cha nyuma lakini kwa kweli tumeshuhudia juhudi kubwa za viongozi wa Serikali, Wizara na TANESCO wanaotutembelea na kutufariji kuwa hali itakuwa shwari, na kweli sasa mambo yameanza kuwa mazuri umeme haukatiki tena mara kwa mara" alisema Mwananchi huyo

Mwenyekiti wa Bodi ya TANESCO Dkt. Alexender Kyaruzi akiongea na wananchi wa Mtama Mkoani Lindi wakati wa ziara ya Bodi ya wakurugenzi wa TANESCO Katika mikoa ya Lindi na Mtwara

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad