HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, December 22, 2017

KANISA LA UKOMBOZI LATEMBELEA KITUO CHA AMANI, LAKUMBUSHA KUJALI WATOTO

WATANZANIA wamekumbushwa kuwajali na kuwangaalia watoto yatima na wale wanaoishi katika mazingira magumu kwa kuwatimizia mahitaji yao ya kimwili na kiroho. Aidha, wamepaswa kutambua kwamba wana wajibu wa kusaidia watoto hao kwa kuwa wanawekeza kwa manufaa ya taifa na wao wenyewe. Kauli hiyo imetolewa na Mwana wa Nabii BG Malisa Mchungaji, Faith Tetemeko wa Kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam, akizungumza baada ya kukabidhi vifaa, bidhaa na mahitaji mbalimbali ya watoto yatima wa kituo cha Amani, kilichopo Bagamoyo, kiasi cha kilomita 65 kutoka Dar es salaam. 
na Mwana wa Nabii BG Malisa Mchungaji, Faith Tetemeko (mwenye gauni la bluu) wa Kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam akizungumza jambo mara baada ya kuwasili kwenye ofisi za Mkurugenzi wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Amani, Margareth Mwegalawa (katikati) kukabidhi vitu mbalimbali kituoni hapo akiwa ameambatana na baadhi ya viongozi wa kanisa, waumini na wamama.
Akitoa maneno yanayogusa nyoyo huku akikariri maandiko Mchungaji Faith alisema:“Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu baba ni hii, kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa” Alifafanua kwamba Kanisa lisiloangalia yatima na wajane si Kanisa, alisema na kuongeza kuwa waumini wanastahili kuwajibika kwa hilo. Aidha, alisema kama Kanisa wanajali watoto na ndio maana wamefunga safari kwenda kuwaona na wamefurahi kuwaona na kushiriki nao tafrija fupi baada ya kuwakabidhi zawadi mbalimbali. na Mwana wa Nabii BG Malisa Mchungaji, Faith Tetemeko (wa kwanza kulia) wa Kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam na baadhi ya viongozi, wakinamama na waumini wakifungua tafrija hiyo fupi kwa maombi kabla ya kukabidhi mahitaji mbalimbali katika kituo cha kulelea watoto yatima kilichopo kijiji cha Zinga, Bagamoyo.[/caption] Waumini wa kanisa hilo walikabidhi mahitaji ya shule ya watoto, mavazi na chakula. Aliwataka watanzania kuwa na tabia ya kujali watoto hao kwa kuhakikisha wanapata mahitaji yao kila siku na sio siku ya sikukuu tu. Alisema watoaji wanapaswa kutoa kwa hali na mali kwa ajili ya kuondoa dhiki za watoto hao, ikiwa ni sehemu ya Baraka kamili kwa Mungu na pia kwa taifa. Alisema watoto hao hawajulikani kesho watakuwa watu gani na kama watalelewa vyema watakuwa ni sehemu ya taifa lenye uadilifu na woga kwa Mungu. [caption id="attachment_3424" align="aligncenter" width="1404"] Baadhi ya wakinamama wa kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam wakishiriki maombi baada ya kuwasili kwenye kituo cha kulelea watoto yatima cha Amani kilichopo katika kijiji cha Zinga, mjini Bagamoyo.[/caption] Alisema kwa kuwezesha utulivu wa watoto hao, watoto watamjua Mungu na hivyo kujenga taifa lenye maisha yenye utukufu wa Mungu. Naye, Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Esther Pilila alisema kwamba kama wanawake katika Kanisa lao wamesukumwa na haja ya kuwaangalia watoto hao kama wajibu wao. Akizungumza kushukuru Mkurugenzi wa kituo hicho Margareth Mwegalawa aliomba watanzania kuwakumbuka watoto hao na kuitafadhalisha serikali kuwapitia kila mara kwa kuwa wao ndio walezi wa watoto. Mwana wa Nabii BG Malisa Mchungaji, Faith Tetemeko wa Kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam akisaini daftari la wageni alipowasili katika kituo cha kulelea watoto yatima cha Amani kilichopo katika kijiji cha Zinga, Bagamoyo.
Alisema pamoja na chakula walichopewa wanatamani watu mbalimbali kuendelea kuwajali watoto kwa kuhakikisha wanakuwa salama. Alisema wadau mbalimbali wasiangalie tu vituo vya mashirika ya dini bali vituo vyote ambavyo vinabeba mzigo wa malezi kwa watoto yatima na wale wanaoishi katika mazingira hatarishi. Alisema kituo cha Amani chenye watoto 40 kinahitaji kupata uzio ili kuhakikisha watoto wapo salama. Mwana wa Nabii BG Malisa Mchungaji, Faith Tetemeko wa Kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam akiwa amempakata mtoto Nicolaus (1.5) wakati wakitazama burudani kutoka kwa watoto wa kituo cha kulelea yatima cha Amani kilichopo katika kijiji cha Zinga, Bagamoyo.  
Naye mtoto Salama Ismail (12) alishukuru kwa misaada hiyo ya mavazi na chakula, mafuta ya kupakaa, miswaki na madaftari na kutaka wananchi wamjue Mungu kwa kuwajali. Naye Haji Joseph (11) aliomba viongozi wa serikali kuwatembelea kwani wao ndio wazazi wao na kuwasaidia kuimarisha upatinakaji wa nishati katika kituo chao hasa umeme wa REA. “Tunaomba viongozi wa serikali watutembelee tuwajue na hasa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa” alisema mtoto huyo. Watoto wa kituo cha kulelea yatima cha Amani kilichopo Zinga, Bagamoyo wakitoa burudani sambamba na Mkurugenzi wa kituo hicho Margareth Mwegalawa walipotembelewa na waumini wa kanisa la Ukombozi wakiongozwa na Mchungaji Faith Tetemeko (hawapo pichani) wakati wa tafrija fupi ya kukabidhiwa mahitaji mbalimbali ya kujikumu kituoni hapo. Pichani juu na chini ni baadhi ya wakinamama wa kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam walioshiriki tafrija hiyo. Mwana wa Nabii BG Malisa Mchungaji, Faith Tetemeko (mwenye gauni la bluu) wa Kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam akicheza sambamba na mtoto Haji Joseph (11) katika tafrija fupi ambapo Kanisa la Ukombozi lilikabidhi vitu mbalimbali zikiwemo sare za shule, vyakula, madaftari, nguo na mahitaji mengine ya kujikimu. Pichani juu na chini ni wakinamama wa kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam wakiwa wamebeba vitu mbalimbali vilivyotolewa kwenye kituo cha watoto yatima cha Amani kilichopo Zinga, Bagamoyo. Mwana wa Nabii BG Malisa Mchungaji, Faith Tetemeko (katikati) wa Kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam akikabidhi vifaa, bidhaa na mahitaji mbalimbali ya watoto wa kituo cha Amani cha watoto yatima, kilichopo Bagamoyo kwa Mkurugenzi wa kituo hicho Bi. Margareth Mwegalawa (kulia) katika hafla fupi iliyofanyika kituoni hapo Bagamoyo. Kushoto ni , Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Kanisa la Ukombozi tawil la Dar es Salaam, Esther Pilila. Mwana wa Nabii BG Malisa Mchungaji, Faith Tetemeko wa Kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa kanisa hilo, watoto pamoja na walezi wa kituo hicho Mwana wa Nabii BG Malisa Mchungaji, Faith Tetemeko wa Kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam katika picha ya pamoja na wakinamama wa kanisa hilo na walezi wa kituo hicho mara baada ya kukabidhi msaada huo. Mwalimu Heavenlight (kushoto) na Mwanaukombozi Favour wakipozi na mtoto Nicolaus (1.5) kuonyesha upendo kwa mtoto huyo Mwana wa Nabii BG Malisa Mchungaji, Faith Tetemeko wa Kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam akigawa chakula kwa watoto yatima wa kituo cha Amani kilichopo Bagamoyo mara baada ya kukabidhi vitu mbalimbali kituo hapo. Watoto yatima wa kituo cha Amani kilichopo Bagamoyo wakifurahia chakula cha pamoja kilichoandaliwa na wakinamama wa kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam. Mwana wa Nabii BG Malisa Mchungaji, Faith Tetemeko wa Kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam akishiriki chakula cha pamoja na watoto yatima wa kituo cha Amani kilichopo Bagamoyo. Mwana wa Nabii BG Malisa Mchungaji, Faith Tetemeko wa Kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam akimlisha chakula mmoja wa watoto yatima wa kituo cha Amani kilichopo Bagamoyo mara baada zoezi la kukabidhi misaada mbalimbali kituoni hapo. Pichani juu na chini ni Wakinamama wa kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam wakicheza michezo mbalimbali na watoto yatima wa kituo cha Amani ukiwemo 'Tulinge Baiyoyo' mchezo ambao katika makuzi kila mtu aliupitia. Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam, Esther Pilila akitoa neno la shukrani kwa uongozi wa kituo hicho mara baada ya kuhitimisha zoezi la kukabidhi msaada huo. Mwana wa Nabii BG Malisa Mchungaji, Faith Tetemeko wa Kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam akizungumza na kituo cha televisheni cha Channel Ten mara baada ya kukabidhi misaada hiyo kituoni hapo. Mtoto Haji Joseph (11) wa kituo cha watoto yatima Amani akitoa neno la shukrani kwa kanisa la Ukombozi kwa kupokea misaada hiyo katika tafrija fupi iliyofanyika kituoni hapo. Mtoto Salama Ismail (12) wa kituo cha watoto yatima cha Amani akitoa shukrani kwa misaada hiyo ya mavazi na chakula, mafuta ya kupakaa, miswaki na madaftari iliyotolewa na wakinamama wa kanisa la Ukombozi tawi la Dar es Salaam. Mkurugenzi wa kituo cha watoto yatima cha Amani kilichopo Bagamoyo, Bi. Margareth Mwegalawa akisisitiza jambo wakati wa mahojiano na waandishi wa habari (hawapo pichani) mara baada ya kupokea msaada huo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad