HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, December 23, 2017

JESHI LA ZIMAMOTO LAFANYA TAMASHA LA UTOAJI ELIMU KWA UMMA

Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Nchini wakionesha utayari wakukabiliana na majanga ya moto.Picha na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji)
Kamishna wa Operesheni wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Billy Mwakatage (Katikati), akizungusha king’ora kama ishara ya Uzinduzi rasmi wa Tamasha la Zimamoto la utoaji elimu kwa niaba ya Kamishna Jenerali wa Jeshi hilo Thobias Andengenye, wakati wa Tamasha la hilo lililofanyika Jijini Dar es Salaam katika viwanja vya Tanganyika Packers vilivyopo eneo la Kawe mapema jana asubuhi tarehe 22/12/2017.

Kamishna wa Operesheni wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Billy Mwakatage, akizungumza na Wananchi wa Jiji la Dar es Salaam wakati wa Uzinduzi rasmi wa Tamasha la Zimamoto la utoaji elimu kwa Umma, wakati wa Tamasha hilo lililofanyika Jijini Dar es Salaam katika viwanja vya Tanganyika Packers vilivyopo eneo la Kawe mapema mapema jana asubuhi tarehe 22/12/2017.

Kamishna wa Operesheni wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Billy Mwakatage (Watatu Kulia), akiwa kwenye banda la mmoja wa mdau aliyeshiriki katika tamasha hilo, wakati wa Tamasha la Zimamoto la utoaji elimu kwa umma lililofanyika Jijini Dar es Salaam katika viwanja vya Tanganyika Packers vilivyopo eneo la Kawe mapema mapema jana asubuhi tarehe 22/12/2017.
Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam Mrakibu wa Zimamoto Peter Mabusi (wanne kushoto) akitoa maelezo kwa Kamishna wa Operesheni Billy Mwakatage (watatu kushoto), Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Benedict Kitalika (Wapili Kushoto), na Kamanda wa Zimamoto Mkoa wa Temeke Laizer Loshpy (kushoto), pindi vikosi mbalimbali vya zimamoto vilivyokuwa vikioonesha zoezi la utayari wakati wa tamasha la Zimamoto na Uokoaji la utoaji elimu lililofanyika katika viwanja vya Kawe Tanganyika Packers mapema mapema jana asubuhi tarehe 22/12/2017.

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA HABARI NA ELIMU KWA UMMA-JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad