HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, December 14, 2017

AGGREY&CLIFFORD YATOA MSAADA KWA KITUO CHA WATOTO WANAOISHI MAZINGIRA MAGUMU, DAR

 Meneja Uhusiano wa kampuni ya Aggrey&Clifford, Martha Majura (kulia) akimkabidhi mkurugenzi wa kituo cha Sadeline Health Care Trust, Sara Kitanda (kushoto) mfano wa hundi ili kusaidia watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu. Wanaoshuhudia kutoka wa pili kushoto ni wakurugenzi watendaji wa Aggrey & Clifford, Luke Smit, Tel Akuku na Ryan Goslin.
 Wafanyakazi wa Aggrey&Clifford wakigawa zawadi na kufurahi na watoto hao.
 Baadhi ya watoto wakiwa na furaha baada ya kupatiwa zawadi na kuonyeshwa faraja na upendo.
Wafanyakazi wa Aggrey&Clifford katika picha ya pamoja na watoto hao wanaolelewa katika kituo cha Sadeline. Kampuni ya Aggrey&Clifford imetoa msaada wa fedha kusaidia kununua mahitaji kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu cha Sadeline Health Care Trust kilichopo Mbezi Beach jijini Dar es Salaam. Mbali na msaada wa fedha, imetoa vifaa vya shule na vyakula ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kusherehekea sikukuu ya Krismasi ambapo pia wafanyakazi wa kampuni walijitolea muda wao kucheza na kufurahi pamoja na watoto hao kwa ajili ya kuwapatia faraja.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad