HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, November 23, 2017

RC GEITA AUNGA MKONO JITIHADA ZA UJENZI WA SHULE NA ZAHANATI KATA YA LUTEDE NA KAKUBILO WILAYANI GEITA

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel ameunga mkono jitihada za ujenzi wa Zahanati na Shule kata za Ludete na Kakubilo Halmashauri ya Geita kwa kuchangia matofali yenye thamani ya shilingi 2,400,000/= na kufanikisha harambee ya mifuko ya Saruji zaidi ya 420.
Mhandisi Robert Gabriel ameunga mkono jitihada za wananchi  baada ya kutembelea kata hizo na kuridhishwa na kazi za ujenzi wa Zahanati za vijiji na Shule zinazofanywa na wananchi kwa kujitolea kufanya kazi bila malipo, kuchangia vifaa mbalimbali vya ujenzi na kuchimba misingi.
Akiwa Kata ya Ludete Mkuu wa Mkoa amesema " Nimefurahi sana kuona namna mnavyoshiriki katika utekelezaji wa miradi hii niwaombe mshiriki kuanzia mwanzo hadi mwisho na msikubali mtu yeyote kuwavunja moyo kwa kuwa maendeleo ya Ludete yataletwa na wananchi wenyewe hivyo mimi ninawachangia matofali 1000 kwa ajili ya Zahanati na mengine 1000 ya kujenga vyumba vya madarasa shule ya Sekondari Ludete".
Awali akimkaribisha Mkuu wa Mkoa Diwani wa Kata ya Ludete Sebastian Benedicto Mranda amesema kuwa wananchi wameamua kujitolea kushiriki  ujenzi wa Shule mpya ya msingi baada ya shule ya Msingi Ludete kuwa na Idadi ya wanafunzi 6,616  huku kukiwa na madarasa 20 yenye mikondo 108 ambao unasababisha msongamano wa wanafunzi darasani. Marando ameongeza kusema kuwa Kata ya Ludete haina Zahanati kwa muda mrefu hivyo wananchi wamejihamasisha kujenga ili wapate huduma katika maeneo yaliyo jirani pia kuunga mkono jitihada za Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Geita kuhakikisha kila kijiji kinakuwa na Zahanati na shule ya msingi na Sekondari kwa Kata, Kata ya ludete ina wanafunzi 900 wanaotarajia kujiunga na elimu ya Sekondari ikiwa na uhaba wa zaidi ya vyumba vya madarasa 20.
Katika ziara hiyo ya Mkuu wa Mkoa amefanya harambee ambayo imefanikisha upatikanaji wa mifuko ya Saruji zaidi ya 420 na kuziagiza Halmashauri kutumia vikundi vya mafundi waliokatika maeneo ya miradi ili kupunguza gharama na kusimamia matumizi ya fedha za miradi hiyo.
Kutokana na Mkoa wa Geita kuwa na uhaba wa vyumba vya madarasa na Zahanati Serikali imeamua kushirikiana na wananchi kufanya kampeni ya mkoa mzima kuhamasisha wananchi kujitokeza kushiriki na kuchangia ujenzi wa miradi ya maendeleo ili wananchi wapate huduma katika majengo bora na mazingira salama.

Mheshimiwa Herman Kapufi Mkuu wa Wilaya ya Geita akitoa maelekezo kwa viongozi wa Halmashauri ya Geita na kata ya kakubilo wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel katika Halmashauri hiyo kuhamasisha ujenzi wa Zahanati na vyumba vya madarasa.

 Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa wa Geita akishirikiana na wananchi wa Kata ya Ludete Wilayani Geita kumwaga zege kwa ajili ya lenta kwenye ujenzi wa madarasa 10 ya shule ya msingi Ludete yenye wanafunzi 6,616  alipokwenda kuzindua kampeni ya ujenzi wa vyumba vya madarasa.





 Mhandisi Robert Gabriel akishirikiana na mafundi kupandisha ndoo yenye zege kwa ajili ya uwagaji wa leta katika majengo 10 ya vyumba vya madarasa shule ya Msingi Ludete Wilayani Geita.

 Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa Geita akikabidhi fedha shilingi 2,400,000/= kwa Diwani wa Kata ya Ludete Sebastian Mranda kwa ajili ya ujenzi wa boma la Zahanati ya Kijiji na Ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari katika hiyo.




 Wananchi wa kijiji cha Ludete Kata ya Ludete Wilayani Geita wakishiriki katika uchimbaji wa msingi kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati katika kijiji hicho kwa lengo la kuunga mkono jitihada za mkuu wa mkoa wa Geita za kila kijiji kuwa na Zahanati.
 Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel akifuatilia kwa karibu maendeleo ya wanafunzi wa kidato cha Tatu shule ya Sekondari Kakubilo Halmashauri ya Geita baada ya kutembelea shule hiyo na kutoa swali la Hisabati kwa wanafunzi hao.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad