HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, November 6, 2017

POLISI KIKOSI CHA RELI ,WANAWAKE DAWATI LA JINSIA WASHEREHEKEA KUANZISHWA KWA MTANDAO NA KUTEMBELEA WATOTO WALIOLAZWA KATIKA TAASISI YA MOYO (JKCI)

 Askari wa Jeshi la Polisi kikosi cha Reli Koplo Grace Ndyamukama akimjulia hali mtoto aliyelazwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) walipotembelea Taasisi hiyo leo  ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwa Mtandao wa Polisi  Wanawake Dawati la Jinsia. Kulia ni Mama wa mtoto Nasra Khalfan.
 Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) ambaye pia ni Mkuu wa kituo cha Polisi Reli Martha Mdinka akimpa zawadi ya dawa ya meno, maji ya kunywa na juisi  Hadija Selemani ambaye amelazwa na mtoto katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) walipotembelea Taasisi hiyo leo  ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwa Mtandao wa Polisi  Wanawake Dawati la Jinsia.
  Askari wa Jeshi la Polisi kikosi cha Reli Rhoda Israel  akimpa zawadi ya juisi  Sada Issah ambaye amelazwa na mtoto katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) walipotembelea Taasisi hiyo leo  ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwa Mtandao wa Polisi  Wanawake Dawati la Jinsia.
 Maafisa wa  Jeshi la Polisi kikosi cha Reli wakigawa zawadi za maji ya kunywa, dawa za mENO,  juisi, mafuta ya kupakaa, sabuni za kuogea na kufulia kwa watoto waliolazwa  katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwa Mtandao wa Polisi  Wanawake Dawati la Jinsia.
 Askari wa Jeshi la Polisi kikosi cha Reli Jane John akimpa zawadi za maji ya kunywa, dawa ya meno,  juisi, mafuta ya kupakaa na  sabuni Maimuna Daud  ambaye amelazwa na mtoto katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) walipotembelea Taasisi hiyo leo  ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwa Mtandao wa Polisi  Wanawake Dawati la Jinsia.
Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) ambaye pia ni Mkuu wa kituo cha Polisi Reli Martha Mdinka akiongea jambo na wagonjwa walipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)  leo  ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwa Mtandao wa Polisi  Wanawake Dawati la Jinsia.
 Maafisa wa  Jeshi la Polisi kikosi cha Reli wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumaliza kutembelea Taasisii ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na kugawa zawadi za maji ya kunywa, dawa za meno,  juisi, mafuta ya kupakaa, sabuni za kuogea  na kufulia kwa watoto waliolazwa  katika taasisi hiyo  ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa kwa Mtandao wa Polisi  Wanawake Dawati la Jinsia.
Picha na JKCI

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad