HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, November 4, 2017

NGULI WA KUPANDA MILIMA KWA BAISKELI DUNIANI, APANDA MLIMA KILIMANJARO

Mpanda milima Mashuhuri kwa kutumia Baiskeli Duniani,Juanito Oiarzabal(katikati) raia wa Ureno na wenzake ,Ramon Abecia (kulia) na Eduardo Pascuaz wakijiandaa kuanza safari ya siku tano kuelekea kilele cha Mlima Kilimanjaro.

Juanito Oiarzabal na wenzake ,Ramon Abecia na Eduardo Pascuaz wakiianza changamoto ya kupanda Mlima Kilimanjaro.
Na Dixon Busagaga, Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.


MPANDA milima Mashuhuri kwa kutumia Baiskeli Duniani,Juanito Oiarzabal raia wa Ureno na wenzake wawili wameanza safari ya siku tano ,kupanda Mlima Kilimanjaro kwa kutumia lango la Kilema ikiwa ni aina mpya ya utalii iliyoanza kushika kasi katika hifadhi hiyo.

Hatua hiyo inatokana na jitihada za shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kueendelea kupanua wigo wa vivutio katika Hifadhi zake 16,kwa kuanzisha aina mpya ya bidhaa za utalii ili kushindana na nchi nyingine duniani katika uuzaji wa safari kwa watalii.

Miongoni mwa bidhaa hizo ni pamoja na zile zilizoanzishwa katika Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimajaro (KINAPA) ya kuzunguka mlima kwa kutumia Parachuti pamoja na kupanda Mlima kwa kutumia Baiskeli, utalii ambao umeanza kushika kasi.

Juanito Oiarzabal ambaye tayari ameweka rekodi nyingi duniani na kuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu kijulikanacho kama World Guinness Book amepanda mlima Kilimanjaro na wenzake wawili ,Eduardo Pascuaz na Ramon Abecia kwa kutumia Baiskeli .

Mkurugenzi wa Utali wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA ) Ibrahim Musa amesema Oiarzabal atakuwa Mreno wa kwanza kuweka rekodi ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa kutumia baiskeli na kwamba aina hi ya utalii na rafiki kwa mazingira ya Hifadhi.

Mkurugenzi wa kampuni ya Safari Bike Africa inayoratibu wa changamoto hii a kupanda Mlima Kilimanjaro kwa kutumia Baiskeli,Mario Martos amesema hatua hii ni mwanzo wa kufungua aina hii ya utali katika Hifadhi za Taifa za Arusha na Saadan.

Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kupitia Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro limeweka utaratibu wa kufanya vipimo kwa wapandaji wa Mlima kwa wanao tumia Baiskeli pia kabla ya kuanza safari ya kuelekea kileleni.

Juanito na wenzake wawili wameianza safari ya siku tano ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa kutumia baiskeli wakipita lango la Kilema ambapo wanatarajia kupita katika Kilele cha Mawenzi kabla ya kuendelea na safari ya kuelekea kilele cha Uhuru.
Mpanda milima Mashuhuri kwa kutumia Baiskeli Duniani,Juanito Oiarzabal(katikati) raia wa Ureno na wenzake ,Ramon Abecia (kulia) na Eduardo Pascuaz wakijiandaa kuanza safari ya siku tano kuelekea kilele cha Mlima Kilimanjaro.
Mpanda milima Mashuhuri kwa kutumia Baiskeli Duniani,Juanito Oiarzabal(katikati) raia wa Ureno na wenzake ,Ramon Abecia (kulia) na Eduardo Pascuaz wakiwa katika picha ya pamoja na Mratibu wa safari hiyo ambaye pia ni mkurugenzi wa kampuni ya Safari Bike Africa ,Mario Martos pamoja na waongoza watalii ,Ally Chuwa na Elvas Mlengwa kabla ya kuanza safari ya siku tano kuelekea kilele cha Mlima Kilimanjaro
Eduardo Pascuaz akifunga kofia ngumu kabla ya safari ya kuelekea Kilele cha Uhuru kuanza.

Muongoza Watalii,Elvas Mlengwa wa kampuni ya Karibu Adventure akishusha Baiskeli maalumu kwa ajili ya zoezi la kupanda Mlma Kilimanjaro.
Baiskeli Maalumu zinazotumika kwa ajili ya kupanda Milima .
Muongoza Watalii ,Ally Chuwa wa Kampuni ya Karibu Adventure akiweka kumbukumbu za vipimo vya mratibu wa Safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa kutumia Baiskeli ,Mario Martos wa Safari Bike Africa kabla ya kuanza kupanda Mlima.
Mmoja wa wageni wanaofanya utalii kwa njia ya Baiskeli ,Ramon Abecia akiandaa baiskeli yake kabla ya kuanza safari ya kuelekea kilele cha Uhuru.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad