HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, November 28, 2017

KATIBU MKUU PROF. ELISANTE OLE GABRIEL ATEMBELEA KIWANDA CHA HUANRI MEDICAL GROUP BEIJING NCHINI CHINA

Katibu mkuu wa  Wizara ya Viwanda ya Biashara na Uwekezaji,  Prof  Elisante   Ole Gabriel  akiwa katika ziara ya kikazi nchini China  (Beijing) ametembelea kiwanda cha  Huanri Medical Group kinachojishughilisha na utengenezaji wa vifaa tiba, Mitungi ya Gesi na Matairi.
Akiwa kiwandani hapo alishuhudia baadhi ya  Vifaa vya tiba vinavyongenezwa kiwandani  hapo Fingertip/Handheld Oximeter ambacho hutumika kupima kiwango cha hewa ya Oxygen katika damu  (vinawafaa zaidi  wakina mama waja wazito na wazee), Anesthesia Machine inayotumika katika upasuaji mkubwa  pale ambapo mtu amewekewa dawa ya usingizi, Ventilator inayotumika ICU kwa ajili ya kusaidia upumuaji kwa mgonjwa aliyezidiwa pamoja na Kifaa kinachofahamika kama Health Machine (Mfano wa Briefcase) kilichotengenezwa mahususi kwa ajili ya soko la  bara la Afrika na kinaweza kutibu takribani magonjwa  16  na kinabeba vifaa vingi ndani yake. 
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda,Biashara na Uwezeshaji Prof. Elisante Ole Gabriel akishiriki katika kuunganisha Mashine inayofahamika kama  "Anesthesia Machine" inayotumika katika usaidizi wa shughuli za  Upasuaji Mkubwa.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwezeshaji Prof. Elisante Ole Gabriel (Katikati) pamoja na ujumbe alioambatana nao, alipotembelea kiwanda cha Huanri Medical Group jijini Beijing nchini China.

 Akieleza lengo la kutembelea kiwanda hicho  Prof. Elisante alisema ni  kuzibaini  fursa za uwekezaji zilizopo na jukumu la wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji ni kuhakikisha kwamba wanajenga mazingira ya  ya wawekezaji  kuwekeza vizuri bila kupoteza muelekeo  na lengo kubwa la kuinua Uchumi wetu. “tungependa tuwe na mikataba ambayo kwa vyovyote vile  hata kizazi kijacho kikija kuangalia hayo makubaliano  kifurahi na kuthamini kwamba  waliongia katika makubaliano waliona mbele na walijali maslahi mapana ya  taifa. 

Tunachoamini  ni kwamba wenzetu hawa wachina  katika tasnia mbalimbali watakuja Tanzania watawekeza,  jukumu letu kubwa sisi  na tunachokifanya ni kuendelea kuwavutia kuwaweka katika mlengo ambao watafanya kazi zao vizuri  katika mazingira wezeshi na rafiki ili mwisho wa siku  ajira ziongezeke  katika nchi yetu ya Tanzania  lakini pia tuweze kuuza vifaa  vingi sana kutoka Tanzania kwenda kwenye masoko ya nje  kwa ajili ya kupata fedha za kigeni  lakini lingine ambalo ni siri kubwa ya mafanikio  ni kupata pia utaalam  ili vijana wa kitanzania waweze kupata taaluma hii  ambayo ni ya kiwango cha  juu”  Alisema Prof. Elisante.
  akifanya mahojiano na vyombo vya habari baada ya kuhitimisha ziara yake kiwandani hapo 
 Akitazama moja ya hatua za kutengenezaji wa Vifaa vya Tiba kiwandani hapo
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Prof. Elisante Ole Gabriel akisalimiana na Rais wa Kampuni ya Huanri Medical Group Bw. Wang qianjun Mara baada ya kuwasili kiwandani hapo.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Prof.Elisante Ole Gabriel akizungumza jambo na Viongozi kutoka China - Asia Economic  Development Association Overseas Cooperation Committee, alioambatana nao Kiwandani hapo.
  Akionyesha furaha yake  Katibu Mkuu  alisema tayari Huanri Medical Group wamekubali walau kwenye masuala ya  taaluma ya vifaa tiba  wataweza kuwaalika vijana wetu wa kitanzania waje wakae China kwa takribani miezi mitatu ili wapate utaalam wa kuunganisha vifaa hivi vya tiba  lakini lengo la serikali yetu ni kuona  kiwanda hiki kikijengwe Tanzania  na hatua hii itapanua wigo wa ajira na pato la taifa litazidi kuongezeka. 

“ Huanri Medical Group  ni miongoni  mwa kundi kubwa la wawekezaji  wanaotarajia kuja  Tanzania Mwezi Machi 2018 kwa ajili  ya mikutano mbalimbali ya uwekezaji  na sisi tunawahakikishia kwamba serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais  Dr. John Pombe Magufuli  inawakaribisha sana, na imani yetu ni kwamba Changamoto ya ajira itaweza kupungua pale tutakapoendelea kuleta wawekezaji nchini.” Alisema  Prof Elisante.
Akihitimisha ziara hiyo katika kiwanda hicho  Prof. Elisante amewataka watanzania kuendelea kupenda vitu vinavyozalishwa katika Taifa letu  na kununua vitu vyetu vya ndani. Amesema  jambo la muhimu na kubwa ni  upatikanaji wa uhamisho wa technolojia kutoka China  na kwamba tayari  Tanzania imeahidi kufanya kazi na wawekezaji  hao  kwa  ushirikiano  kwa lengo la  kuhakikisha ndoto na falsafa hii ya serikali ya awamu ya tano  inakamilika na kufikiwa kwa  kwa kasi nzuri.”

Kwa upande wake Rais wa kampuni hiyo ya Huanri Medical Group Bw. Wang qianjun amefurahishwa na juhudi ambazo zinafanywa na Serikali ya Tanzania kwenye sekta ya viwanda  na ameahidi ushirikiano mkubwa na  kuonyesha utayari wake wa kuwekeza Tanzania . 
Katika ziara hiyo Katiba Mkuu  wa Wizara ya  Viwanda,Biashara na Uwekezaji Prof. Elisante Ole Gabriel aliambatana na Afisa Mwandamizi wa Ubalozi wa Tanzania nchini China Said Massoro, Viongozi kutoka  China - Asia Economic Development  Association Overseas Cooperation  Committee (Naibu Katibu Mkuu Bi.  Rui LU na Makamu wa Rais Bi. Tian Wenhui) Bw.Remidius Emmanuel  Katibu Mkuu wa  Shirikisho la Wanafunzi Watanzania nchini China pamoja  Bi. Muka Kamuzora  Mtanzania anayesoma  Masuala ya Uchumi hapa China.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad