HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, November 23, 2017

BARAZA LA MADIWANI MKURANGA LAAZIMIA KUBORESHA MIUNDO MBINU

 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mkuranga,  Juma Abed akizungumza na waandishi habari mara baada ya kuahirisha kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika mapema wiki hii kikiwa na lengo la kujadili mikakati ya kimaendeleo ya Mkuranga.


Baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Mkuranga limeitaka wakala wa Barabara mijini na vijijini (Tarura) kushirikiana na halmashauri na viongozi wa ngazi za chini katika kuboresha miundombinu ya barabara katika maeneo husika.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya baraza la  Madiwani la halmashauri ya  mkuranga mwenyekiti wa baraza hilo, Juma Abed amesema tarura imekua ikifanya kazi zake bila kuwashirikisha madiwani hali ambayo inasababisha utendaji na utekelezaji wa miradi ya barabara kutotekelezeka kwa wakati.

Aidha Abed amesema kuwa miradi ya ujenzi wa miundombinu  ya barabara ijengwe imara na kuachana na biashara ya ujenzi wa kila mwaka.
 Mkurugenzi wa halmashauri ya Mkuranga, Mshamu Munde akizungumza juu ya mikakati ya Halmashauri hiyo ikiwemo kuboresha miundo mbinu.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mkuranga, Juma Abed akiwa katika picha ya pamoja madiwani, watendaji wa Halmashauri.picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad