HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, October 20, 2017

VETA CHANG'OMBE YAPEWA MSAADA WA MAGARI TISA YA KUFUNDISHIA

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
CHUO cha Ufundi Cha VETA Chang'ombe  kimepata msaada wa magari tisa kutoka katika shirika la Elizabeth Glasser Padiriatic  Foundation (EGPAF) yatakayotumika kwa ajili kujifunzia wanafunzi katika chuo hicho.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Mkurugenzi wa Kanda ya Dar es Salaam, Habib Bukko amesema kuwa msaada wa magari ni mkubwa kutokana na changamoto walikuwa wanakabiliana nayo.

Bukko amesema kuwa chuo cha ufundi  kimekuwa hakina magari ya kutosha kwa ajili ya kujifunzia na taratibu za serikali zinataka magari yanunuliwe mapya lakini msaada huo ni hatua moja nzuri ya kusaidia chuo hicho.

Amesema kuwa watu wengine wenye mashirika wanaweza kuwasaidia magari yao ambayo wanataka kuyauza kwani kwao ni msaada mkubwa kutokana na mahitaji yaliyopo katika zaidi vyuo 700 vya ufundi.

Aidha ameesma kuwa zaidi vijana milioni 25 wanahitaji kupata mafunzo hivyo kuna umhimu wa kuwa rasilimali ya vifaa katika kuweza kuendana na idadi hiyo.

 Nae Mkurugenzi wa Uendeshaji wa  EGPAF, Jacquesdol Massawe amesema kuwa wanatambua umhimu magari hayo kwa ajili ya kuwafundishia vijana wakitanzania na kuweza kupata ujunzi na kuja kutumika katika uzaslishaji.

Amesema uchumi wa viwanda unahitaji kuwa rasilimali watu wenye ujuzi kuweza kutumika katika uzalishaji wa viwanda hivyo.
 Mkurugenzi wa Kanda ya Dar es Salaam wa VETA, Habib Bukko akizungumza na waandishi habari juu ya msaada wa magari tisa yalitolewa na Shirika la EGPAF leo jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Uendeshaji wa EGPAF, Jaccquesdol Massawe akizungumza juu ya msaada  magari tisa jinsi yatavyotumika katika kufundishia vijana vyuo vya VETA, leo jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Chuo cha VETA Changombe,  Douglas Kipokola akizungumza namna ya kuyatumia magari hayo katika chuo hicho leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Kanda ya Dar es Salaam wa VETA, Habib Bukko akipokea nyaraka za magari hayo kutoka kwa Mkurugenzi wa Uendeshaji wa EGPAF, Jaccquesdol hatika hafla iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya magari tisa yaliyotolewa na shirika la EGPAF.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad