HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, October 18, 2017

TATUMZUKA YAWEKA HISTORIA KWA KUTOA MILIONI 150 KUPITIA DROO YA SUPA MZUKA ‘JACKPOT’

 
 Afisa Mkuu wa Masoko, wa Tatu Mzuka Sebastian Maganga akifafanua jambo mapema leo mchana,wakati akieleza namna Supa Mzuka Jackpot inavyofanyika na namna mshindi anavyopatikana.Maganga alisema

"Kwa Sasa kila wakati ukicheza Tatu Mzuka hadi tarehe 19 Novemba, unapata bure nafasi ya kujishindia Tzs.150 milioni za uhakika kupitia droo ya Supa Mzuka Jackpot" alisema na kuongeza kuwa Wiki iliyopita Juma Othman (pichani kushoto),aliibuka mshindi wa Mzuka Jackpot na kujinyakulia kitita cha Tz.55 milioni.
Pichani kulia ni Juma Othman mwenye umri wa miaka 21 tu, akitoa ushuhuda namna alivyoshinda Mzuka Jackpot na kujinyakulia kitita cha Tz.55 milioni. Mshindi huyo ambaye anaishi na mama yake wilayani Bagamoyo, aliishukuru Tatu Mzuka huku akibainisha kuwa ushindi huo umebadilisha maisha yake.
  Afisa Mkuu wa Masoko, wa Tatu Mzuka Sebastian Maganga akimkabidhi mfano wa hundi Juma Othman aliyeibuka mshindi wa Mzuka Jackpot na kujinyakulia kitita cha shilingi milioni 55 za Kitanzania.

 
Tatu Mzuka kwa mara nyingine wamevunja rekodi kwa kuwaletea Watanzania jackpot kubwa zaidi kuwahi kutokea nchin. 

Donge nono la shilingi milioni 150 litatolewa kwa mshindi mmoja atakayebahatika siku ya tarehe 19 Novemba 2017, kupitia droo ya Supa Mzuka Jackpot.

Kupitia Supa Mzuka Jackpot, Watanzania wanashinda mara 1, si 2 bali nafasi 3 za kushinda kiasi kikubwa cha pesa kwa bei ya soda!

Njia tatu za kushinda na Tatu Mzuka ni;
1) Kushinda hadi milioni 6 kila saa, masaa 24 kwa siku

2) Kushinda Sh100,000,000 kupitia Mzuka Jackpot Jumapili hii, saa 9:30 usiku.

3) Kushinda Tzs.150,000,000 kupitia Supa Mzuka Jackpot tarehe 19 Novemba
Sebastian Maganga, Afisa Mkuu wa Masoko, wa Tatu Mzuka alielezea namna Supa Mzuka Jackpot inavyofanyika.

"Kwa Sasa kila wakati ukicheza Tatu Mzuka hadi tarehe 19 Novemba, unapata bure nafasi ya kujishindia Tzs.150 milioni za uhakika kupitia droo ya Supa Mzuka Jackpot" ilifafanua Maganga.

Wiki iliyopita Juma Othman, mshindi wa Mzuka Jackpot aliondoka na Tz.55 milioni. Othman mwenye umri wa miaka 21 tu, ambaye anaishi na mama yake wilayani Bagamoyo, aliishukuru Tatu Mzuka kwani ushindi huo umebadilisha maisha yake.

Tatu Mzuka imebadili maisha ya Watanzania hakika,hadi sasa imetengeneza mamilionea Zaidi ya 70 na kutoa zaidi ya bilioni 3 kwa zaidi ya washindi milioni 1 na laki tatu.

Homa ya Tatu mzuka inapoendelea kupanda, swali linabaki kuwa je? Nani ataondoka na donge kubwa Zaidi katika historia ya Tanzania.




No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad