Na Agness Francis, Blogu ya Jamii.
Waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano, Prof Makame Mbalawa amehudhuria hafla ya kusaini kwa mkataba na mkandarasi wa mradi wa ujenzi wa reli ya kati ya kisasa itumiayo umeme kwa kiwango cha Standard gauge ambapo itaanzia kipande cha Morogoro hadi Makutopora .
Hafla hiyo ya utiaji saini ya makubaliano ya ujenzi iliyofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam ambapo kilometa 336 ni za njia kuu na kilometa 86 ni za njia za kupitishia treni na maeneo ya kupangia mabehewa jumla yake ni kilometa 422
Kampuni hodhi ya rasilimali za reli Tanzania (RAHCO) inaendeleza kutekeleza ahadi za ujenzi wa reli hiyo ikiwa awamu ndogo ya kwanza ujenzi wa kipande kidogo cha Dar es Salaam hadi Morogoro (KM205) utekelezaji wake umekwishaanza.
Katika utekelezaji wa awamu ya pili kati ya zile tano ambazo zinaendelezwa hadi kufikia Mwanza ujenzi huo una gharimu takribani dola za kimarekani 1,923,695,000.
Waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano, Prof Makame Mbalawa ameishukuru kampuni ya RAHCO pamoja na Kampuni ya Yapi Merkezi kutoka nchini Uturuki kwa kazi kubwa wanayoifanya katika utelelezaji huo wa awamu ya 1 na ya 2
Vile vile Prof. Mbalawa amepongeza serikali ya awamu ya 5 kwa kuupa kipaumbele kikubwa mradi huu wa reli ya umeme kiwango cha Standard gauge ya kisasa, hata hivyo amesema kuwa kukamilika wa mradi huo ita punguza gharama za usafiri kwa wafanyabiashara .
Mjumbe wa Bodi ya Kampuni ya Yapi Merkezi, Erdem Arioglu na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya ( RAHCO) Masanja Kadogosa na Mjumbe wa Bodi ya Kampuni ya Yapi Merkezi, Erdem Arioglu wakisaini mkataba mpya wa ujenzi wa reli mpya ya kisasa ya umeme ya Standard gauge katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Kampuni hodhi ya rasilimali za reli Tanzania (RAHCO) na TRL, Masanja Kadogosa na Mjumbe wa Bodi ya Kampuni ya Yapi Merkezi ya Nchini Uturuki, Erdem Arioglu wakionyesha mikataba hiyo mara baada ya kumaliza kusaini leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbalawa akizungumza na wageni waalikwa pamoja na kutoa pongezi za dhati kati ya kampuni hizo mbili kwa hatu waliyofikia hadi sasa makubaliano hayo ya saini ya ujenzi wa wa reli ya kati kwa kiwango cha Satandard gauge kati ya kampuni ya (RAHCO) pamoja na Yapi Markezi ya Uturuki leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam. Picha na Agness Francis, Blogu ya Jamii.
No comments:
Post a Comment