HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, September 9, 2017

Tamasha la Efm Njendani lakonga nyoyo za mashabiki wao Kigamboni.

Na Agness Francis, Blogu ya Jamii.
Kituo cha radio cha Efm kimewatembelea wakati wa Kigamboni  pamoja na kufanya vipindi moja kwa moja kupitia radio hiyo na kusikiliza changamoto mbalimbali za wakazi na kuzifanyia utatuzi ukiwa pia lengo ni kuwa karibu na wasikilizaji wao.

Tamasha hilo la  muziki Mnene Njendani limehudhuriwa na Mkuu wa wilaya Kigamboni Hashim Mgandilwa, Mkurugenzi Manispaa ya Kigamboni Stephen  Katemba wakiambatana na Mstahiki Meya wa Dar es Salaam Isaya Mwita ili kuweza kuongea na wananchi moja kwa moja kupitia Kituo cha radio cha Efm katika Viwanja vya Machava  Kigamboni Jijini Dar es Salaam.

Viongozi nao wa meweza kuzungumza na wakati wa Manispaa kisikiliza kero na changamoto zinazowakabili wananchi nao wa Kigamboni waliojitokeza kwa wingi katika Viwanja hivyo.

Vile vile pia kituo hicho kimelenga hasa kukuza vipaji chipikizi vya miziki maarufu kwa jina la  Singeli, kwa kufanya mashindano  na kwa atakae ibuka Kidedea kati ya washiriki nao atapata fursa ya  kurekodi kazi zake bure  kwa gharama za kituo hicho cha redio ya Efm.
 Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni  Hashim Mgandilwa(kushoto)  akisalimiana na Mstahiki Meya wa Dar es Salaam  Isaya Mwita(kulia)  katika tamasha hilo la Muziki  Mnene njendani lililokuwa linafanyika kwenye Viwanja vya Machava Kigamboni.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni,  Stephen Katemba akizungumza na wakazi wa Kigamboni katika kipindi cha Joto la  asubuhi ambacho kilirushwa moja kwa moja  kutoka  Viwanja vya Machavya wilaya ya Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Watangazaji wa kipindi cha joto  la asubuhi  wakiongozwa na Gerard Hando pamoja na Maulid Kitengewakirusha kipindi hicho  mubashara  kutoka katika Viwanja vya Machava Kigamboni.
 Watangazaji wa kipindi cha uhondo wakiongozwa na Dina Marius  wakirusha kipindi hicho  mubashara kutoka wiwanjani hapo sambamba na kutoa burudani kwa mashabiki wao waliojitokeza  kwa wingi katika Tamasha Njendani Viwanja vya Machava wilaya ya Kigamboni jijini Dar  es salaam.
 Mtangazaji wa kipindi cha Sport HQ, Tunnu Shenkome akizungumza na  mashabiki wa timu ya Yanga Fc, Simba Fc  pamoja na Azam Fc wakionyeshana tambo kila mmoja  akijinadi kuwa timu yake ndio itakayoibuka kidedea kunyakua  kombe hilo la VPL katika msimu huu.
 Msanii wa muziki wa Singeli,  Dogo Niga  akitoa burudani kabambe kwa wakazi wa Kigamboni katika tamasha la  Njendani lililofanyika kwenye Viwanja vya Machava Kigamboni.
Mashabiki wa Efm watu wazima kwa watoto  walijitokeza kwa wingi kupata burudani pamoja na kuonana na Watangazaji mbalimbali  wa kipindi vya radio hiyo katika tamasha la  Njendani lililofanyika kwenye Viwanja vya Machava Kigamboni. (Picha na Na Agness Francis, Blogu ya Jamii)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad