Na Agness Francis, Blogu ya Jamii.
Mradi wa kuimarisha
mifumo ya elimu katika nchi za Afrika mashariki (SESEA)
ambazo ni Tanzania, Kenya na Uganda imehitimisha mafunzo yake kupitia chuo kikuu cha Agha Khan katika wilaya ya Kilwa mkoani Lindi.
Hafla hiyo iliofanyika katika Halmashauri
ya Kilwa mkoani Lindi ambao mradi huo unoafadhiliwa na Global Affairs
Cannada pamoja na Agha Khan Foundation unaolenga kuongeza taaluma
kwa walimu wa shule za awali na
za msingi ili kufikia idadi kubwa ya
wasomi nchini.
Akizungumza Mkurugenzi wa Elimu ya juu, Wizara ya Elimu, Sayansi, teknolojia na mafunzo ya Ufundi, Profesa Sylvia Temu katika hafla hiyo ya kuhitimisha
mafunzo hayo amesema kuwa ushirikishwaji kwa wazazi na
jamii kwa njia ya warsha na
semina umesaidia kuongeza ushiriki
katika kusaidia kuleta matokeo chanya ya elimu kwa watoto wa kike na wa kiume na imesaidia
kuweza kutunga vitabu vya hadithi
kwa lugha ya Kiswahili, na kiingereza
na kaika nukta nundu kwa kuzingatia mazingira yao.
Hata hivyo Slyvia Temu
amesema kuwa kupitia mbinu ya Education
Community of Practice mradi umeshirikiana na Halmashauri kuanzaisha jumuiya za kitaaluma za walimu 1,200 kwenye shule zote 150,
jumuiya hizi huwai hukutana shuleni na kwenye klasta zao kuimarisha utaalamu wa
kufundishia mbinu mpya ya kusoma kwa kujifunza (Reading to learn) ikiwa
miongoni mwa walimu zaidi 750 waliopata mafunzo
hayo na mradi uliwaongezea
maarifa walimu 307 wanaume wakiwa ni 179 na wanawake ni 128 ili kuwafanya walimu wawe imara zaidi.
Nae mwakilishi wa
mkuu wa chuo cha Agakhan, Mkurugenzi wa mradi Nicolaus
Washira amesema kuwa SESEA lengo lake ni kutaka kuinua na kuimarisha Elimu nchini pamoja na kuongeza wigo la wasomi kwa kutembelea wilaya 4 ambazo ni
Klwa, Nachingwea, Newala pamoja na Lindi Vijijni.
Vilevile Mkurugenzi wa mradi, Bernard Orimbo amesema kuwa
;bila kupata Elimu huwezi kupata
maendeleo na ili nchi iweze kupata
mafanikio huwezi kutumia bunduki
bali elimu ndio hupaswa kuwa stari wa mbele; amesema Mkurugenzi huyo.
Mkurugenzi wa Elimu ya juu, Wizara ya Elimu, Sayansi, teknolojia na mafunzo ya Ufundi, Profesa Sylvia Temu akizungumza na walimu wa Shule za msingi ambapo walimu walifanya maonesho ya zana za vitendo ambazo hutumika katika kufundishia wanafunzi pindi wanapokuwa masomoni katika Halmashauri ya Kilwa mkoani Lindi. Profesa Slyvia Temu alimwakilisha wa Katibu mkuu Wizara elimu, sayansi na teknolojia, Dkt Leonard Akwilapo.
Wanafunzi wa Shule za msingi waliojitokeza katika hafla
hiyo wakisikiliza namna jinsi SESEA inavyotoa huduma ya Elimu na umuhimu wake katika Halmashauri ya
Kilwa mkoani Lindi.
No comments:
Post a Comment