HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, September 11, 2017

RAIS MAGUFULI AGOMA KUPEWA ORODHA YA WAFUNGWA WANAOTAKIWA KUNYONGWA

Rais John Pombe Magufuli amefunguka na kutoa kauli yake kuhusu baadhi ya wafungwa ambao wamehukumiwa kunyongwa kutokana na makosa mbalimbali na kudai kuwa yeye anaogopa kusaini ili wafungwa hao wanyongwe.

Rais Magufuli amesema hayo leo Ikulu jijini Dar es Salaama wakati akimuapisha Jaji Mkuu wa Tanzania Prof. Ibrahim Hamis Juma na kusema anatambua kuwa idadi wa wafungwa waliohukumiwa kunyongwa ni wengi sasa ila anaomba asipewe hiyo orodha.

"Sisi wanasiasa tunaogopa kunyonga, natambua kuwa sasa orodha ya watu ambao wanatakiwa kunyongwa ni kubwa sana ila mimi naomba hiyo orodha msiniletee kwa sababu najua ugumu wake ulivyo" alisisitiza Rais Magufuli

Mbali na hilo Rais Magufuli amesema kuwa amechukua muda mrefu kumteua Jaji Mkuu wa Tanzania kutokana na ukweli kwamba alikuwa anatafuta mtu ambaye anaweza kuendana na dhamira yake ya kupambana na rushwa hivyo alipojilidhisha na jaji huyo ndiyo maana ameamua kumteua kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad