HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, September 20, 2017

PICHA: TETEMEKO LAUWA WATU 250 WAKIWEMO WATOTO 20 NCHINI MEXICO



Tetemeko kubwa la ardhi limeikumba Mexico na kuua watu karibu 250 na kuangusha makumi ya majengo katika mji mkuu wa Mexico City.


Rais Enrique Peña Nieto amesema zaidi ya watoto 20 wamekufa na 30 hawajulikani walipo baada ya jengo la shule kuanguka.


Tetemeko hilo la ardhi lenye ukubwa wa alama 7.1 limesababisha uharibifu mkubwa katika majimbo ya jirani na Mexico City.
   Jengo la ghorofa likiwa limetiti kufuatia kutokea kwa tetemeko nchini Mexico
                   Waokoaji wakiendelea na shughuli ya uokoaji kwa kufukua vifusi vya majengo
 Miili ya watu waliokufa kwa tetemeko ikiwa imelazwa na kuwashiwa mishumaa katika kuomboleza.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad