HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, September 6, 2017

MKUU WA WILAYA KIBAHA ASSUMPTER MSHAMA AFUNGA MACHINJIO YA PANGANI KIBAHA KWA MUDA USIOJULIKANA

MKUU wa Wilaya  ya Kibaha  Mkoani Pwani  Bi Assumpter Mshama  ametoa amri ya kufungia  machinjio mapya yaliyopo  Mtaa wa Mtakuja Pangani  Kibaha  Mkoani Pwani kwa muda usiofahamika  kutokana na kukithiri kwa uchafu  unaotishia  afya za walaji  wa eneo  la Kibaha na Vitongoji vyake

Bi Assumpter ametoa amri hiyo muda mfupi uliopita baada ya kufanya ziara ya kushtukiza machinjioni hapo.

Aidha  Bwana Afya Ramadhan Mohammed  ambaye husimamia  shughuli za machinjio hayo amekiri  kuwa  machinjio hayo yanakabiliwa na changamoto nyingi  ikiwa hi pamoja na ukosefu wa maji na umeme.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad