HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, September 27, 2017

MKUTANO WA MAJAJI NA MAHAKIMU WAFUNGWA LEO JIJINI DAR LEO.


Rais wa Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania Mhe. Jaji Ignas Kitusi akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kufunga mkutano Mkuu wa Majaji na Mawakili wa wanachama wa Jumuiya ya Madola.
Waziri wa Katiba Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Haroun Ally Suleiman, akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufunga mkutano Mkuu wa Majaji na Mawakili uliokuwa ukifanyika jijini Dar es Salaa kuanzia Septemba 25-28, 2017 Ambpo alifunga Mkutano huo kwa niaba ya Rais wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein.
 Wawakili na Majaji wakiwa katika Mkutano wa mwaka ya wanachama wa Jumuiya ya madola jijini Dar es Salaam leo.
 Picha na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.

RAIS wa Chama cha Majaji na Mahakimu Tanzania, Jaji Ignas Kitusi amesema, Serikali inamchango mkubwa katika kuiwezesha mahakama  kutimiza majukumu yake ili iweze kusonga mbele katika maendeleo, 
huku majaji na mahakimu wakizungumzia miiko ya utendaji kazi mahakama.

Jaji Kitusi amesema hayo leo wakati wa ufungaji wa mkutano mkuu wa mwaka wa majaji na mahakimu wa Jumuiya ya madola uliomalizika leo jijini Dar es Salaam.

amesema kuwa,  katika mkutano huo wamejadili mbalo mbali moja wapo zikiwa ni changamoto wanazokutana nazo mahakimu na Majaji zikiwepo changamoto za kimtandao, usafirishaji wa binadamu ambayo pia ni changamoto.

Amesema ili kujua kama kila mwanachama wa mkutano huo amezingatia maazimio waliyofikia, mkutano mwingine mkubwa utafanyika nchini Australia ili kujipima ambapo moja kati ya maazimio waliyofikia ni  kuzingatia miiko ya kazi na kiutendaji kwa ujumla, "kwani  kila nchi imetengeneza sheria na vitabu vyake vya kanuni na maadili vinavyoongoza majaji na mahakimu.

Aidha amesema kuwa, katika mkutano huo pia wamezungumzia changamoto za ucheleweshaji wa mashauri na kuongeza kuwa kwa kuiga nchi mbali mbali ambazo zimefanya vizuri katika sekta hiyo, ni wazi kuwa nchi ambazo ziko nyuma zitaiga mfano Wa nchi hizo ili kupunguza msongamano wa mashauri mahakamani.

. Changamoto ya kifedha ambayo inahitaji ushiriki Wa serikali katika kuwezesha mahakama kutimiza majukumu yaliyopo, maadili, rasilimali watu.

alisema kuwa, kuna changamoto nyingi zinazowakabili mahakimu au majaji zikiwemo za kimaadili na kutoa wito kwa Jamii nzima kuiacha mahakama ifanye kazi bila kuiingilia na pia majaji na mahakimu wafanye kazi kwa kuzingatia sheria na ushahidi bila kuruhusu kuingiliwa na vishawishi kwa namna yoyote.

Aidha alisema, Serikali inaowajibu wa kuangalia kazi za majaji na mahakimu kwani kazi zao mara nyingine zinawaweka hatarini, na ni jukumu la serikali kutoa hali ya usalama kwao Ili waweze kusikiliza kesi zao bila ya kuwa na wasiwasi na usalama wa maisha yao.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad