Waziri
wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Prof. Makame Mbarawa
akiongea na Balozi wa Ufaransa nchini, Bi. Malika Berak mara baada ya kuwasili
kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere katika Kongamano la
Kwanza la Kitaifa la Usafiri wa Anga lililoanza leo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Prof. Makame Mbarawa (mwenye tai nyekundu waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki wa Kongamano la Kwanza la Usafiri wa Anga linalofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere. Kushoto kwa Waziri ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Salim Msangi na kulia Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), Bw. Hamza Johari.
.
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
SERIKALI imesema kuwa inatatizo la
mabaruni wa kurusha ndege hali ambayo inahitaji kusomesha marubani kwa wingi na
kuacha kuchukua nje ya nchi.
Hayo ameyasema Waziri wa Ujenzi,
Mawasiliano na Uchukuzi, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa wakati wa ufunguzi wa
mkutano wa sekta ya usafiri wa Anga leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini
Dar es Salaam.
Mbarawa amesema kuwa sasa ni wakati
wa kusomesha marubani, mafundi pamoja wahandisi wa ndege kutokana na mahitaji
ya hao wote katika kufikia uchumi wa kati wa 2025.
Amesema kuwa hakuna sababu ya watu
hao kuchukua nje ya nchi wakati malengo ya serikali kwenda kwa kasi katika
maendeleo ya sekta ya usafiri wa anga ambayo ndiyo itafanya kuongeza kwa pato
la taifa pamoja na uchumi.
Mbarawa amesema kuwa serikali
imejipanga katika ujenzi wa miundombinu ikiwemo miundombinu ya viwanja vya
ndege katika na kuweza kufanya Tanzania kuwa kiunganishi kwa safari za ndege za
nchi mbalimbali.
Aidha amesema kuwa wanahitajika
wawekezaji makini katika sekta ya usafiri wa anga na sio wawekezaji wa kufanya
blablaa na kufanya sekta hiyo ishindwe kukua kwa kasi katika malengo ya
serikali.
Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Hamza Johari amesema
kuwa mkutano huo utajadili mada mbalimbali ikiwemo kupungua kwa shehena katika
viwanja vya ndege pamoja na bidhaa zinazozalishwa nchini kutumia viwanja nchi
jirani ambapo wadau ndio wenye majibu ya kuweza kuitatua changamoto hiyo.
Johari amesema kuwa katika mkutano huo ni muhimu katika sekta ya usafiri
anga katika kuboresha huduma ili iweze
kwenda kwa kasi katika ukuaji wa uchumi.
Nae Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la
Ndege Nchini (ATCL), Ladislaus Matinde amesema mahitaji ya ndege duniani 39620
kwa Afrika ni 10150 huku marubani
617000 duniani na Afrika 22000 na
Mafundi 814000, Afrika Mafundi wa Ndege 24000.
No comments:
Post a Comment