HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, September 25, 2017

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA MKUTANO WA MWAKA WA MAJAJI NA MAHAKIMU WA JUMUIYA YA MADOLA JIJINI DAR ES SALAAM LEO.

Na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.
MAKAMU wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Hassan Suluhu leo amefungua mkutano Mkuu wa Mwaka wa chama cha majaji na mahakimu wa Jumuiya ya Madola  katika ukumbi wa mkutano wa Benki Kuu (B.O.T) jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo ambao umezinduliwa leo Septemba 25 hadi,2017  amnbao utafanyika kwa siku tatu ukiwa na kauli mbiu isemayo 'Mahakama Madhubuti, inayowajibika na Jumuishi'. ambapo kutakuwa na maada mbalimbali kutka kwa viongozi ambao ni Majiji na mahakimu.

Akizungumza mara baada ya kufungua mkutano huu Mwenyekiti wa Chama cha Mawakili Tanzania, Ignas Hatusi amesema kuwa Mkutano huo una lengo la Kujenga mahakama shirikishi, mahakama inayowajibika na mahakama Dhabiti kiutendaji  kwa kuimarisha utendaji wa taasisi za kimahakama.

Pia amesema wanachama hao wa jumuiya ya madola watajifunza kutoka kwa majaji na mahakimu mbalimbali kutoka nchi mbalimbali za jumuiya ya hiyo na ikiwa pamoja kutoa huduma bora kwa wananchi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano wa Mwaka wa chama cha majaji na mahakimu wa Jumuiya ya Madola  unaoendelea kufanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu jijini Dar es Salaam kwa siku tatu mfurulizo ambapo kauli mbiu ya Mkutano huo ni  'Mahakama Madhubuti, inayowajibika na Jumuishi'.Mkutano huo umehudhuriwa na majaji pamoja na mahakimu wa nje mwanachama wa Jumuiya ya Madola.
Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma  akizungumza katika Mkutano wa Mwaka wa chama cha majaji na mahakimu wa Jumuiya ya Madola  unaofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Benki kuu (B.O.T) jijini Dar es Salaam kwa siku tatu Mfurulizo Mkutano huo unakauli mbiu inayosema  'Mahakama Madhubuti, inayowajibika na Jumuishi'.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Majaji pamoja na mahakimu wanawake waliohudhuria mkutano Mkuu wa Mwaka wa Majaji na mahakimu wa Jumuiya ya Madola Unaofanyika jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Mikutano wa Benki kuu (B.O.T) leo Septemba 25, 2017 hadi Septemba 28, 2017.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa katiika picha ya pamoja na majaji na mahakimu waliohudhuria mkutano Mkuu wa Mwaka wa Majaji na mahakimu wa Jumuiya ya Madola Unaofanyika jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Mikutano wa Benki kuu (B.O.T) leo Septemba 25, 2017 hadi Septemba 28, 2017.
 Bendi ya Jeshi la Polisi wakiimba wimbo wa Taifa katika mkutano wa Majaji na Mahakimu unaofanyika katika ukumbi wa Benki Kuu ambao umejumuisha wajaji na mahakimu wa wa nchi mwanachama wa jumuiya ya madola.
 Kwa heshima wakimba wimbo wa Taifa wakiongozwa na bendi ya Jeshi la Polisi leo katika ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Jajaji na Mahakimu wa Jumuiya ya Madola.


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan  akiteta jambo na Jaji Mkuu, Profes Ibrahim Juma leo kabla ya kufungua mkutano mkuu wa Mwaka wa Majaji na Mahakimu unaofanyika katika ukumbi wa Mkutano wa Benki Kuu jijini Dar es Salaam leo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad