Wahitimu
24 katika shule ya Msingi Jeshi la Wokovu wakitumbuiza katika mahafari
yao ya Kuhitimu Masomo ya Shule ya Msingi jijini Dar es Salaam leo.
VIFIJO
na ndelemo vilivyochangamana na majozi kwa wanafunzi wanaohitimu masomo
yao ya shule ya msingi katika shule ya watoto wenye ulemavu ya Jeshi la
Wokovu jijini Dar es Salaam leo.
Furaha
iliyoje kwa watoto waliohitimu masomo ya msingi na majozi kwa
waliobakia, ikiwa risala ya wahitimu imetoa changamoto mbalimbali kwa
watoto wenye ulemavu ikiwemo vifaa visaidizi kwa watoto hao pamoja na
mafuta ya kupaka kwa watoto wenye ulemvu wa ngozi(Albino).
Akizungumza
katika mahafali hayo jijini Dar es Salaam leo, Mwalimu wa Michezo
katika shule ya Msingi Jeshi la Wokovu, Emmanuel Ibrahim ameiomba
serikali kuwaruhusu watoto hao wenye ulemavu na wanavipaji mbalimbali
washiriki mashindano ya Kitaifa pamoja na ya kimataifa kama watoto
wengine.
Pia
wameomba kuongezewa Madaktari watakaotoa huduma ya afya kwa watoto hao
wenye ulemavu ilikukidhi mahitaji ya watoto wenyeulemavu shuleni hapo.
Mkurugenzi wa shule ya msingi ya Jeshi la wokovu iliyopo Tameke jijini
Dar es Salaam, Luteni Thomas Sinana akisoma risala ya shule hiyo kwa
mgeni rasmi na kutaja changamoto mbalimbali zinazoikabiri shule hiyo
inayohudumia watoto walemavu katika hafla ya mahafali ya wanafunzi wanao
hitimu masomo yao ya shule ya msingi jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi wa shule ya msingi ya Jeshi la wokovu iliyopo Tameke jijini Dar es Salaam, Luteni Thomas Sinana akimkabidhi Mgeni
Rasmi katika mahafali ya shule ya msingi ya watoto wenye ulemavu
mbalimbali, Kamishina wa ustawi wa Jamii, Rabikira Mushi katika hafla ya wanafunzi wa Darsasa la Saba 2017 jijini Dar es Salaam
leo.
Mgeni Rasmi
katika mahafali ya shule ya msingi ya watoto wenye ulemavu
mbalimbali, Kamishina wa ustawi wa Jamii, Rabikira Mushi akizungumza na
watoto pamoja na wazazi katika hafla ya wanafunzi wa Darsasa la Saba
2017 jijini Dar es Salaam
leo. Pia amesema changamoto mbalimbali zilizotajwa kati Risala ya watoto
hanaohitimu zitashughulikiwa.
Katibu
wa Kanisa la Jeshi la waokovu, Luteni Kanali Samweli Mkami akizungumza
na wahitimu pamoja na wazazi wenye watoto walemavu wasiwafiche waende
katika shule ya jeshi la wokovu ili kujipatia malezi mazuri pamoja na
elimu katika shule hiyo.
Watoto
wenye ulemavu wakitoa burudani mbele ya Mgeni rasmi pamoja na wazazi wa
watoto hao waliohudhuria katika mahafali ya wanafunzi wa Darsa la saba
2017 jijini Dar es Salaam leo.
wahitimu
wa shule ya msingi Jeshi la Wokovu na Watoto wenye ulemavu tofauti
tofauti wakitumbuiza ngojera mbele ya mgeni rasmi zilizokuwa na mahusia
mazuri kwa wazazi wenye watoto wenye ulemavu pamoja na kuwashuru walezi
na walimu wao kwa kuwalea tangu walipokuwa Darsa la kwanza mapaka sasa
wanahitimu masomo yao ya shule ya msingi.
Wahitimu wa Shule ya Msingi Jeshi la wokovu wakimsiliziza mgeni rasmi jijini Dar es Salaam leo wakati wa mahafali ya kuwaaga.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Shule ya msingi ya watoto wenye ulemavu ya Jeshi la
wokovu iliyopo Temeke Jijini Dar es Salaam, Neema Urio akizungumza kwa
niaba ya Kamati ya shule na kuwashukuru walezi wa watoto wenye ulemavu
katika shule hiyo jijini Dar es Salaam leo katika mahafari ya kuhitimu
Msomo ya Shule ya Msingi ya wanafunzi 24 .
Mwenyekiti
wa Kamati ya Shule ya msingi ya watoto wenye ulemavu ya Jeshi la
wokovu iliyopo Temeke Jijini Dar es Salaam, Neema Urio akiwa na Mwalimu
wa Mazoezi katika shule ya Msini Jeshi la Wokovu, Emmanuel Ibrahim
katika mahafari ya Wanafunzi wa Darasa la saba wanao hitimu masomo yao
ya shule ya msingi.
Burudani
ikiendelea kati ya wazazi na watoto wenye ulemavu katika mahafali ya
shule ya Msingi Jeshi la Wokovu jijini Dar es Salaam leo.
Mmoja
ya wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi akimsaidia mwenzake Mwenye ulemavu
wa Viungo katika Mahafali ya Wahitimu wa Darasa la saba 2017 katika
shule ya Msingi Jeshi la wokovu Jijini Dar es Salaam.
Wahitimu
wa Masomo ya Shule ya Msingi katika shule ya Jeshi la wokovu jijjini
Dar es Salaam wakisoma risala mbele ya Mgeni rasmi.
Baadhi
ya walimu na walezi wa wanafunzi walemavu wa shule ya msingi Jeshi la
waokovu wakiwa katika mahafali ya wanafunzi 24 waliohitimu masomo yao ya
shule ya Msingi.
Bendi ya Jeshi ikitumbuiza katika mahafili ya wanafunzi wanaohitimu masomo yao ya shule ya msingi jijini Dar es Salaam leo.
Wahitimu
wa masomo ya Darasa la Saba katika shule ya Msingi Jeshi la Wokovu
wakitoa zawadi kwa waliimu wao pamoja na walezi wao kwa kuwajua sauti
zao pamoja na matendo ambayo huwafanyia watoto hao pia kwa kuwaita kwa
kuigiza sauti zao.
Mgeni
Rsmi akipokea zawadi kutoka kwa wahitimu wa Darsa la saba katika shule
ya Msingi Jeshi la Wokovu jijini Dar es Salaam leo.
Wakati kutoa zawadi na vyeti kwa wahitimu wa shule ya Msingi Jeshi la waokovu jijini Dar es Salaam leo.
Picha zote na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
No comments:
Post a Comment