HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, September 9, 2017

MAHAFALI YA SHULE YA MSINGI YA WATOTO WALEMAVU YA JESHI LA WAOKOVU JIJINI DAR ES SALAM LEO.

 Wahitimu 24 katika shule ya Msingi Jeshi la Wokovu wakitumbuiza katika mahafari yao ya Kuhitimu Masomo ya Shule ya Msingi jijini Dar es Salaam leo.
VIFIJO na ndelemo vilivyochangamana na majozi kwa wanafunzi wanaohitimu masomo yao ya shule ya msingi katika shule ya watoto wenye ulemavu ya Jeshi la Wokovu jijini Dar es Salaam leo.

Furaha iliyoje kwa watoto waliohitimu masomo ya msingi na majozi kwa waliobakia, ikiwa risala ya wahitimu imetoa changamoto mbalimbali kwa watoto wenye ulemavu ikiwemo vifaa visaidizi kwa watoto hao pamoja na mafuta ya kupaka kwa watoto wenye ulemvu wa ngozi(Albino).

Akizungumza katika mahafali hayo jijini Dar es Salaam leo, Mwalimu wa Michezo katika shule ya Msingi Jeshi la Wokovu, Emmanuel Ibrahim ameiomba serikali kuwaruhusu watoto hao wenye ulemavu na wanavipaji mbalimbali washiriki mashindano ya Kitaifa pamoja na ya kimataifa kama watoto wengine.

Pia wameomba kuongezewa Madaktari watakaotoa huduma ya afya kwa watoto hao wenye ulemavu ilikukidhi mahitaji ya watoto wenyeulemavu shuleni hapo.
Mkurugenzi wa shule ya msingi ya Jeshi la wokovu iliyopo Tameke jijini Dar es Salaam, Luteni Thomas Sinana akisoma risala ya shule hiyo kwa mgeni rasmi na kutaja changamoto mbalimbali zinazoikabiri shule hiyo inayohudumia watoto walemavu katika hafla ya mahafali ya wanafunzi wanao hitimu masomo yao ya shule ya msingi jijini Dar es Salaam leo.
  Mkurugenzi wa shule ya msingi ya Jeshi la wokovu iliyopo Tameke jijini Dar es Salaam, Luteni Thomas Sinana akimkabidhi Mgeni Rasmi katika mahafali ya shule ya msingi ya watoto wenye ulemavu mbalimbali, Kamishina wa ustawi wa Jamii, Rabikira Mushi katika hafla ya wanafunzi wa Darsasa la Saba 2017 jijini Dar es Salaam leo.
Mgeni Rasmi katika mahafali ya shule ya msingi ya watoto wenye ulemavu mbalimbali, Kamishina wa ustawi wa Jamii, Rabikira Mushi akizungumza na watoto pamoja na wazazi katika hafla ya wanafunzi wa Darsasa la Saba 2017 jijini Dar es Salaam leo. Pia amesema changamoto mbalimbali zilizotajwa kati Risala ya watoto hanaohitimu zitashughulikiwa.
 Katibu  wa Kanisa la Jeshi la waokovu, Luteni Kanali Samweli Mkami akizungumza na wahitimu pamoja na wazazi wenye watoto walemavu wasiwafiche waende katika shule ya jeshi la wokovu ili kujipatia malezi mazuri pamoja na elimu katika shule hiyo.
Watoto wenye ulemavu wakitoa burudani mbele ya Mgeni rasmi pamoja na wazazi wa watoto hao waliohudhuria katika mahafali ya wanafunzi wa Darsa la saba 2017 jijini Dar es Salaam leo.
wahitimu wa shule ya msingi Jeshi la Wokovu na Watoto wenye ulemavu tofauti tofauti wakitumbuiza ngojera mbele ya mgeni rasmi zilizokuwa na mahusia mazuri kwa wazazi wenye watoto wenye ulemavu pamoja na kuwashuru walezi na walimu wao kwa kuwalea tangu walipokuwa Darsa la kwanza mapaka sasa wanahitimu masomo yao ya shule ya msingi.
 Wahitimu wa Shule ya Msingi Jeshi la wokovu wakimsiliziza mgeni rasmi jijini Dar es Salaam leo wakati wa mahafali ya kuwaaga.
Mwenyekiti wa Kamati ya Shule ya msingi  ya watoto wenye ulemavu ya Jeshi la wokovu iliyopo Temeke Jijini Dar es Salaam, Neema Urio akizungumza kwa niaba ya Kamati ya shule na kuwashukuru walezi wa watoto wenye ulemavu katika shule hiyo jijini Dar es Salaam leo katika mahafari ya kuhitimu Msomo ya Shule ya Msingi ya wanafunzi 24 .
 Mwenyekiti wa Kamati ya Shule ya msingi  ya watoto wenye ulemavu ya Jeshi la wokovu iliyopo Temeke Jijini Dar es Salaam, Neema Urio akiwa na Mwalimu wa Mazoezi katika shule ya Msini Jeshi la Wokovu, Emmanuel Ibrahim katika mahafari ya Wanafunzi wa Darasa la saba wanao hitimu masomo yao ya shule ya msingi.


 Burudani ikiendelea kati ya wazazi na watoto wenye ulemavu katika mahafali ya shule ya Msingi Jeshi la Wokovu jijini Dar es Salaam leo.
 Mmoja ya wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi akimsaidia mwenzake Mwenye ulemavu wa Viungo katika Mahafali ya Wahitimu wa Darasa la saba 2017 katika shule ya Msingi Jeshi la wokovu Jijini Dar es Salaam.
 Wahitimu wa Masomo ya Shule ya Msingi katika shule ya Jeshi la wokovu jijjini Dar es Salaam wakisoma risala mbele ya Mgeni rasmi.


 Baadhi ya walimu na walezi wa wanafunzi walemavu wa shule ya msingi Jeshi la waokovu wakiwa katika mahafali ya wanafunzi 24 waliohitimu masomo yao ya shule ya Msingi.
 
 Bendi ya Jeshi ikitumbuiza katika mahafili ya wanafunzi wanaohitimu masomo yao ya shule ya msingi jijini Dar es Salaam leo.
 Wahitimu wa masomo ya Darasa la Saba katika shule ya Msingi Jeshi la Wokovu wakitoa zawadi kwa waliimu wao pamoja na walezi wao kwa kuwajua sauti zao pamoja na matendo ambayo huwafanyia watoto hao pia kwa kuwaita kwa kuigiza sauti zao.













 Mgeni Rsmi akipokea zawadi kutoka kwa wahitimu wa Darsa la saba katika shule ya Msingi Jeshi la Wokovu jijini Dar es Salaam leo.

 Wakati  kutoa zawadi na vyeti kwa wahitimu wa shule ya Msingi Jeshi la waokovu jijini Dar es Salaam leo.





















Picha zote na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad