HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, September 3, 2017

KATIBU MKUU WA WIZARA YA AFYA NA MAENDELEO YA JAMII,BI.SIHABA NKINGA AFUNGUA MKUTANO WA REPSSI JIJINI ARUSHA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Watoto, Bi Sihaba Nkinga akizungumza katika mkutano wa kimataifa wa watoto ulioandaliwa na taasisi ya REPSSI yenye makao yake nchini Afrika Kusini kutoka mataifa zaidi ya 30 barani Afrika unaofanyika jijini Arusha,mkutano huo pamoja na mambo mengine unalenga kuwawezesha watoto sauti zao kusikika na kuwajenga kisaikolojia.
Afisa Mtendaji Mkuu wa taasisi ya REPSSI, Noreen Huni ambaye ni raia wa Zimbabwe akizungumza katika mkutano huo wa kimataifa jijini Arusha leo.
Watoto kutoka mataifa mbalimbali wakifatilia mada kwenye mkutano huo.
Watoto kutoka mataifa mbalimbali wakiwa kwenye mkutano ambao unawapa fursa ya kuwasilisha taarifa za matukio ambayo ni changamoto kwao.
Watoto wakiwa kwenye mkutano ambao unawapa fursa ya kuwasilisha taarifa za matukio ambayo ni changamoto kwa mamlaka husika na kutafutiwa ufumbuzi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wanawake na Watoto,Bi Sihaba Nkinga(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa baraza la watoto nchini,Joel Festo(kushoto) na Mwenyekiti wa baraza la watoto nchini Kenya,Brian Musyoka katika mkutano wa kimataifa wa watoto ulioandaliwa na taasisi ya REPSSI yenye makao yake nchini Afrika Kusini .
Mmoja wa washiriki akifatilia kwa makini.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wanawake na Watoto,Bi Sihaba Nkinga(katikati)akiagana na viongozi wa watoto mara baada ya kufungua mkutano huo jijini Arusha.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad