HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, September 5, 2017

IDRIS SULTAN AZINDUA VIATU VYAKE

 Mshindiwa Big brother Afrika 2014 Idris Sultan amezindua viatu vyake viitwavyo SULTAN by FOREMEN akiwa pamoja na klabu ya GENTLEMAN ya Jack Daniel. Uzinduzi huu ulifanyika pamoja kama namna ya kuwaunganisha wanaume wa Tanzania kuwa sehemu ya viatu hivi maalum na umoja endelevu.
 SULTAN by FORMEN ni chapa ya viatu iliyotengenezwa kwa kuzingatia unadhifu, ubora, starehe (comfort) na hadhi ya uzito wa viatu vya mwanaume wa kitanzania.
“Tumetengeneza dizaini tofauti zit akazoingia sokoni kubadilisha ulimwengu wa fasheni katika usafi, unadhifu, furahanauchangamfu. Aina hii ya viatu inawakilisha mwanaume wa kitanzania anayefanya kazi zake kwa bidii, kwa ubunifu akiwa na muonekano wa tofauti unaopendeza” asema Idris.
 Chapa hii ya SULTAN by FOREMEN ni mafanikio mapya kwa Idris ukiacha mafanikio yake mengine aliyoyapata hivi karibuni kama kuchaguliwa kuigiza katika movie ya Hollywood marekani itakayogharimu takribani dola million 5. 
Idris ambaye alifanikiwa kukonga nyoyo za mashabiki wa filamu Tanzania baada ya kushiriki katika filamu ya KIUMENI ambayo imeshinda tunzo mbili katika tamasha la filamu la ZIFF
Idris ni mchekeshaji na kijana maarufu anayependa kuvaa vizuri na kwenda na wakati hivyo atauza viatu hivi kwa bei nafuu ilikila mtanzania aweze kuvimudu.
 Uzinduzi huu wa viatu vya SULTAN klabu ya GENTLEMAN ya Jack Daniel ulibarikiwa na viongozi wa serikali, wanamzuziki, wanamitindo, wabunifu, waigizaji na watu wengi mashuhuri.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad