Mwenyekiti wa Chama cha Viziwi Tanzania (Chavita) Nidrosy Mlawa
akizungumza na waandishi habari juu ya changmoto ya viziwi katika
upatikanaji wa taarifa pamoja na mawasiliano katika jamii kwa kusaiadiwa
na Mkalimani Octavian Simba hayupo pichani leo jijini Dar es Salaam.
katika kufanya utendaji katika maeneo wa ser
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
CHAMA Cha Viziwi Tanzania (Chavita) kimesema kuwa viziwi wanakabiliwa na changamoto kwenye shughuli za maendeleo ya jamii katika nyanja za siasa na kiuchumi kutokana na ulemavu huo kwa kuwa kikwanzo katika mawasiliano na upatikanaji wa habari katika jamii hiyo .
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Chama hicho, Nidrosy Mlawa amesema kutokana na changamoto zinazowakabili watu wasiosikia wanatarajia kuendesha mradi katika mikoa mitatu katika kutoa mafunzo kwa watendaji wa serikali za mitaa juu kutambua haki za watu wasiosikia.
Mradi huo utaendeshwa kwa kipindi cha miezi sita katika Mikoa ya Morogoro, Mwanza pamoja na Arusha ambapo watakutana na watendaji wa serikali za mitaa katika mikoa hiyo na kupata taarifa mbalimbali zinahusiana viziwi juu ya changamoto ya mawasiliano pamoja na utumiaji wa lugha za alama katika shule ambazo zina watoto viziwi.
Mlawa amesema mradi huo utagharimu sh. Milioni 80 ambazo wamepata ufadhili na The Foundation For Civil Society katika kugusa changamoto za viziwi ikiwemo kwa watendaji wa serikali za mitaa kutambua na kufanya ufatiliaji wa matumizi ya mafungu ya fedha zinazotengwa kwa ajili ya watu wenye Ulemavu katika Halmashauri zao.
Aidha amesema kuwa Chavita kikipata ushirikiano katika mradi huo kwa watendaji katika mikoa hiyo ili kufanya Jamii ya Tanzania kuwa jamii juu jumuishi.
Amesema kuwa sekta ya elimu haina walimu hawajui lugha ya alama na kusababisha wanafunzi viziwi kutopata elimu bora kama sera ya elimu ya 2004 inavyoanisha.
No comments:
Post a Comment