HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, September 14, 2017

BASATA yazungumzia umuhimu wa masomo ya sanaa mashuleni Kisarawe.

Na Agness Francis, Blogu ya Jamii.
Wanafunzi 100  wahitimisha mafunzo ya sanaa ikiwa ni mara ya pili  kufanyika   katika halimashauri ya wilaya ya kisarawe Mkoani Pwani,ikishirikisha  shule 5 kutoka  katika wilaya hiyo ambazo ni Chanzige A,ChanzigeB,Kibasila,Kazimzumbwi  pamoja  na Sanze .

Nae muwakilishi wa  mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Simon  Biginagwa amezungumza  hayo leo katika Halimashauri ya wilaya ya Kisarawe  Mkoa wa Pwani  amesema  kuwa sasa ni wakati wa kuendeleza utamaduni wetu wa kitanzania  badala  ya  tamaduni na mila za kizungu akiongezea kuwa  kupia tamaduni zetu hupata fursa ya kuweza  kupa ajira na amesisitiza pia kulinda amani  nchini  .

Hata hivyo Mkurugenzi Ukuzaji  Sanaa na Masoko Basata  Vivian Shalua amemshukuru mkuu wa wilaya ya kisarawe kwa kuwapa kibali cha kuweza  kufanya mafunzo ya sanaa kwa  wanafunzi hao na  ;NIvizuri watoto  kufanya sanaa wakiwa mashuleni na Lengo ikiwa ni  kukuza viapaji vya watoto na kufufua ngoma zetu za utamaduni;  amesema Mkurugenzi huyo.

Afisa  elimu  Halimashauri  ya kisarawe  Zipporah Daniel  Simwanza, amewapongeza basata kwa  kuweza kurudi tena katika Halmashauri hiyo  kuweza kufanya zoezi hilo la uandaaji wa kutoa mafunzo ya sanaa  kwa wanafunzi hao .

Vilevile  Afisa maendeleo ya jamii  Halimashauri ya Kisarawe Wanchoke Juma ametoa wito kwa walimu kufundisha  watoto  mafuzo ya sanaa  mashuleni na kulichukulia somo la sanaa kama masomo mengine badala ya kulifanya kama la ziada.
Mkurugenzi Ukuzaji  Sanaa na Masoko Basata  Vivian Shalua, akizungumza na wanafunzi wa shule  za Kisarawe juu ya umuhimu wa kuendeleza sanaa na  tamaduni za  kitanzania leo katika Halimauri ya Kisarawe Mkoani pwani.
Afisa Elimu Halimashauri ya Kisarawe, Zipporah Daniel Simwanza akizungumza na wanafunzi wa  Halimashauri ya Kisarawe na kuwapongeza kwa kujitokeza kwa wingi katika  kupata mafunzo ya sanaa yalioandaliwa na Basata na kuwataaka wanafuzi hao kudumisha tamaduni zetu leo katika Halimashauri ya mji wa Kisarawe  Mkoa wa Pwani.
 Mwakilishi wa  mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Simon  Biginagwa, akizungumza na wanafunzi hao akiwataka  pia kuendeleza utamaduni wetu badala ya kuiga ule wa kizungu kwani sanaa ni chanzo cha ajira na kutoa wito kwa wazazi kuwaruhu watoto kushiriki mafunzo  hayo ya sanaa leo katika hafla ya kuhitimisha mafunzo hayo  Halmashauri ya Kisarawe Mkoani Pwani
Baadhi ya wanafunzi wa Shule za msingi za Kisarawe wakitoa burudani ya kuimba na kucheza  ya ngoma za asaili  mojawapo kati ya mafunzo waliyopata kwa viongozi,  waandishi wa habari  pamoja na walimu wao leo katika hafla ya kuhitimisha mafunzo hayo  Halmashauri ya Kisarawe Mkoani Pwani  .
Picha ya pamoja wakiwepo viongozi wa Kisarawe waandaaji wa mafuzo hayo Basata pamoja na walimu waliofundisha saana hizo mbalimbali ikiwemo kuimba, kucheza nyimbo za tamaduni ya asili ya Mtanzania leo katika hafla ya kuhitimisha mafunzo hayo  Halmashauri ya Kisarawe Mkoani Pwani. (Picha na Agness Francis, Blogu ya Jamii)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad