Waziri
Mkuu Kassim Majaliwa (kulia) akisalimiana na Balozi wa Cuba Nnchini
Tanzania Bwana Lucas Domingo Polledo walipo kutana kwa mazungumzo ya
kikazi jana August 22/2017 akiwa katika ziara ya kikazi Havana Cuba. Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu.
WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Cuba
nchini Tanzania, Balozi Lucas Domingo Polledo, ambapo amewakaribisha
wafanyabiashara wa Cuba kuja kuwekeza katika ujenzi wa viwanda vya
dawa.
Amesema
kwa sasa Serikali ya Tanzania inaagiza dawa kutoka nje ya nchi jambo
ambalo linasababisha kutumia fedha nyingi, hivyo uwepo wa kiwanda
utasaidia katika kupunguza gharama. Pia wawekezaji watakuwa na uhakika
wa soko la bidhaa zao.
Waziri
Mkuu aliyasema hayo jana jioni (Jumanne, Agosti 22, 2017) wakati
akizungumza na Balozi Polledo mjini Havana. Waziri Mkuu yuko nchini Cuba
kwa ajili ya ziara ya kikazi yenye lengo la kudumisha ushirikiano kati
ya nchi hizo mbili.
Alisema
Serikali imedhamiria kuendeleza sekta ya viwanda nchini kama mkakati wa
kukuza uchumi na kufikia uchumi wa kati, hivyo wafanyabiashara kutoka
nchini Cuba wanakaribishwa kuja kuwekeza nchini, hususani katika viwanda
vya dawa na sukari.
Waziri
Mkuu alisema licha ya Tanzania kuwa ni nchi ya amani na yenye utulivu
wa kisiasa, pia imeweka mazingira mazuri ya uwekezaji jambo ambalo
litawawezesha watakaokuja kuwekeza nchini kupata tija.
No comments:
Post a Comment